Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA aliuliza:- Wilaya ya Serengeti ni kitovu cha utalii na ni Wilaya inayopata watalii wengi lakini haina Hospitali ya Wilaya na hivyo kuleta usumbufu kwa wageni pamoja na wakazi wa Serengeti:- Je, ni lini Hospitali ya Wilaya itakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nina maswali mawili ya nyongeza.
La kwanza tarehe 24 Mei, 2017 wakati Naibu Waziri akijibu swali langu lililokuwa linahusu kupeleka dawa kwenye vituo vya afya niliuliza swali la nyongeza lililokuwa linahusu hospitali hii ya Wilaya. Bahati nzuri Naibu Waziri amefika kwenye hospitali ile akaona, alisema kwamba wametenga shilingi milioni 700 kwenda kumalizia OPD ambayo hiyo ingekuja kabla ya mwaka wa fedha 2016/2017 haujaisha. Mwaka wa fedha 2016/2017 umeisha. Alitamka kwenye Bunge hili, wananchi wa Serengeti walisikia zinaenda shilingi milioni 700 kumalizia OPD. Je, alilidanganya Bunge na wananchi wangu wa Serengeti? Kama siyo kwamba alidanganya, nini kilitokea?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, mantiki ya kupeleka fedha Serengeti ilikuwa siyo kulidanganya Bunge na zoezi hili tutalifanya maeneo mbalimbali. Kama Serikali, tuna mpango na tumezungumza kwamba katika programu ya Serikali kwamba tutafanya katika sekta ya afya hasa vituo vya afya vile ambavyo vimeonekana ni changamoto kubwa katika maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha sasa, takribani vituo 142 tutavifanyia ujenzi huo ambayo ni equivalent pesa yake karibuni shilingi milioni 700 katika kila center kwa ajili ya kutengeneza miundombinu na kupeleka vifaa tiba.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kudanganya Bunge, jambo hilo halipo isipokuwa ni commitment ya Serikali. Kwa hiyo, jambo la msingi ni kwamba watu wa Serengeti wavute subira kwa sababu Serikali ina mipango yake na inatekeleza.
Katika ujenzi huu sehemu nyingine tunafanya bulk procurement kuufanya ujenzi huu tupate mkandarasi wa pamoja kuhakikisha ujenzi huu unaenda sambamba katika maeneo yote na lengo letu kwamba tupate value for money na ubora wa majengo ule unaokusudiwa tuweze kuupata vizuri. Kwa hiyo, ni commitment ya Serikali kuhakikisha kwamba inapeleka huduma za afya kwa wananchi wake wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Name

Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA aliuliza:- Wilaya ya Serengeti ni kitovu cha utalii na ni Wilaya inayopata watalii wengi lakini haina Hospitali ya Wilaya na hivyo kuleta usumbufu kwa wageni pamoja na wakazi wa Serengeti:- Je, ni lini Hospitali ya Wilaya itakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza kwa Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo lililopo Serengeti linafanana na tatizo lililopo Manispaa ya Moshi na ukizingatia kwamba Manispaa ya Moshi ndiyo Makao Makuu ya Mkoa wa Kilimanjaro na ndiyo eneo ambalo watalii wote wanaoenda mlima Kilimanjaro hupitia pale. Tumekuwa na ombi la muda mrefu la kuomba Hospitali ya Wilaya Serikalini kwa zaidi ya miaka sita au saba hapa. Swali langu, je, Serikali itatusaidia lini kutekeleza ombi letu maalum la kujenga Hospitali ya Wilaya katika Manispaa ya Moshi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli inawezekana kulikuwa na maombi maalum katika vipindi mbalimbali, lakini tufahamu kwamba haya maombi maalum mara nyingi sana siyo kama ile bajeti ya msingi. Kwa hiyo, inategemea kwamba ni jinsi gani Serikali kipindi hicho imepata fedha za kutosha ku-accommodate maombi maalum.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, najua kwamba Moshi kweli hakuna Hospitali ya Wilaya, lakini ukiangalia vipaumbele vya Taifa hili hata ukiangalia katika maeneo mengine kwa mfano kama Serengeti alipokuwa anazungumza ndugu yangu Mheshimiwa Marwa pale, wako tofauti sana na Moshi. Angalau Moshi mna alternative pale, watu wanaweza wakaenda KCMC au sehemu nyingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tutaangalia jinsi tutakavyofanya. Ninyi kama Halmashauri ya Wilaya anzeni kufanya hiyo resource mobilization katika ground level na sisi tutaangalia jinsi gani tulifanye jambo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, ndiyo maana katika kusaidia katika suala zima la Moshi kwa ujumla wake (Moshi Mjini na Vijijini) sasa hivi tunaenda kukiboresha kituo cha Uru Mashariki pale. Lengo kubwa ni kwamba kiweze kusaidiana na hospitali zile ambazo ziko pale kwa lengo kubwa lile lile la kuwasaidia wananchi wa Moshi waweze kupata huduma nzuri ya afya.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA aliuliza:- Wilaya ya Serengeti ni kitovu cha utalii na ni Wilaya inayopata watalii wengi lakini haina Hospitali ya Wilaya na hivyo kuleta usumbufu kwa wageni pamoja na wakazi wa Serengeti:- Je, ni lini Hospitali ya Wilaya itakamilika?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri alifika Jimboni kwangu na amekiona Kituo cha Dongobesh na tukaleta ombi la kujengewa theater, je, Mheshimiwa lini sasa theater ile inajengwa ili wananchi wangu wapate matibabu hayo ya upasuaji? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tuliweza kufika Dongobesh na kuweza kufanya tathmini ya changamoto kubwa inayokabili huduma ya afya katika eneo lile.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mpango wa Serikali ndiyo nimezungumza katika vituo 142 kwamba na Dongobesh ni miongoni mwa kituo ambacho tunaenda kukijengea theater; lakini siyo theater peke yake; tutajenga pale theater tutaweka na vifaa lakini halikadhalika tutaweka uboreshaji wa miundombinu kwa bajeti iliyotengwa pale Dongobesh. Kwa hiyo, naomba niwatoe hofu wananchi wa Dongobesh kwamba jambo hili kwa sababu manunuzi yake tumepeleka kwa ujumla, tufanye subira, ni commitment ya Serikali kwamba siyo muda mrefu sana kazi hii itaanza mara moja.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA aliuliza:- Wilaya ya Serengeti ni kitovu cha utalii na ni Wilaya inayopata watalii wengi lakini haina Hospitali ya Wilaya na hivyo kuleta usumbufu kwa wageni pamoja na wakazi wa Serengeti:- Je, ni lini Hospitali ya Wilaya itakamilika?

Supplementary Question 4

MHE.VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri kwanza nimpe pongezi kubwa kwa kazi kubwa ambayo ametufanyia pale Kilolo kwa ujenzi wa hospitali, ni kilio cha muda mrefu. Pamoja na hayo, bado shida ipo, tuna tatizo kubwa sana la wagonjwa ambao inabidi waende kutibiwa kwenye Kituo cha Kidabaga lakini kituo kile kiko mbali na kata kama Idete, Masisiwe, Boma la Ng’ombe na Kata nyingine. Tatizo ni kwamba hakipo sawasawa kwa sababu hakuna daktari, hakuna chumba cha upasuaji, hakuna wodi ya akina mama wala hakuna ambulance. Sasa kwa wakati huu tunaposubiria ile hospitali, unasemaje?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika Halmashauri ya Kilolo, kwanza walikuwa hawana Hospitali ya Wilaya, lakini namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge, tulipofika pale tulifanya initiatives za kutosha na walipata karibu shilingi bilioni 2.2. Wao ni miongoni mwa watu wanaojenga hospitali ya kisasa sasa hivi, nawapongeza sana kwa kazi kubwa inayoendelea kufanyika pale. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo najua kwamba kutoka pale kwenda Kidabaga ni mbali sana na ndiyo maana Serikali katika kipindi cha sasa tutaenda kufanya ule ujenzi. Nilishamweleza Mheshimiwa Mbunge kwamba wananchi wa Kidabaga wawe na amani, kituo chao ni miongoni mwa vituo tunaenda kufanyia uboreshaji mkubwa kwa sababu kijiografia eneo lile lina changamoto kubwa sana. Time frame yetu tuliyoweka ni kwamba kabla ya mwezi wa Disemba kituo kile kitakuwa kimekamilika na facilities zake zote. (Makofi)