Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 3 Public Service Management Ofisi ya Rais TAMISEMI. 24 2016-04-21

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU (K.n.y. JOSEPH K. MUSUKUMA) aliuliza:-
Hospitali ya Geita imefanywa kuwa Hospitali ya Mkoa tangu tarehe 8 Januari, 2016:-
Je, ni lini DMO aliyekuwa akiongoza Hospitali hiyo atahamia katika hospitali iliyopendekezwa na kikao cha RCC kuwa Hospitali ya Wilaya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Kasheku Musukuma, Mbunge wa Geita, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, licha ya kupandisha hadhi ya Hospitali ya Wilaya ya Geita kuwa Hospitali ya Mkoa lakini bado inaendelea kuwa ya Wilaya hadi tarehe 1 Julai, 2017 itakapokabidhiwa rasmi. Hivyo, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Geita (DMO) bado anaendelea kuwa msimamizi wa hospitali hii hadi kipindi hicho itakapohamia rasmi ngazi ya Mkoa na kusimamiwa na Mganga Mkuu wa Mkoa.
Mheshimiwa Spika, halmashauri inaendelea na taratibu za kupendekeza kituo cha afya ambacho kitapandishwa hadhi kuwa Hospitali ya Wilaya katika kipindi cha mpito wakati taratibu za kujenga Hospitali ya Wilaya zinafanyika. Natoa wito kwa halmashauri kuwasilisha pendekezo hilo mapema katika vikao vya kisheria ili liweze kujadiliwa na hatimaye kuwasilishwa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ili kupata ridhaa.