Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU (K.n.y. JOSEPH K. MUSUKUMA) aliuliza:- Hospitali ya Geita imefanywa kuwa Hospitali ya Mkoa tangu tarehe 8 Januari, 2016:- Je, ni lini DMO aliyekuwa akiongoza Hospitali hiyo atahamia katika hospitali iliyopendekezwa na kikao cha RCC kuwa Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 1

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, katika Kituo cha Afya cha Nzela ambacho kimekuwa kikihudumia wananchi wa Jimbo la Geita na ni kikubwa na tayari kimekwishafanyiwa maamuzi na Halmashauri ya Wilaya. Je, Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari kuambatana na Mheshimiwa Mbunge kwenda katika kituo hicho na kuona kama kinafaa kufanywa kuwa Hospitali ya Wilaya?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, baada ya Hospitali ya Geita ambayo ndiyo ilikuwa Hospitali ya Wilaya kuwa Hospitali ya Mkoa, hivi sasa kuna vifaa vingi ambavyo zimeletwa na Mkoa lakini hakuna Madaktari na watumishi mbalimbali. Je, lini Mheshimiwa Waziri atapeleka watumishi na watalaam katika Hospitali ya Wilaya ya Geita?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote, nipende kuwapongeza Wabunge wote wa Geita kwa kazi kubwa waliyoifanya kwa kushirikiana na Geita Gold Mine (GGM) kwa kuhakikisha kwamba Hospitali yao ya Wilaya ya Geita imekuwa na structure ambayo inarahisisha sasa kufanya hospitali hiyo kuweza kutoa huduma bora. Nishukuru sana kwa sababu tulikuwa na Makamu wa Rais pale na Waziri mwenye dhamana wa sekta ya afya na kushuhudia hospitali ile kukabidhiwa vile vifaa kwa kweli tunawapongeza sana kwa kazi kubwa mliyoifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, jinsi gani ya kuambatana nami, naomba nikiri wazi mchakato huu wa Bunge la Bajeti ukiisha nilikuwa na ziara maalum ya Mkoa wa Geita, hili litakuwa ni miongoni mwa eneo moja ambalo tutakwenda kulifanyia kazi kwa pamoja. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, suala zima la kupatiwa wataalam, naomba niwajulishe ndugu zangu si muda mrefu mtasikia sasa Wizara ya Afya inatoa idadi ya waajiriwa katika sekta hiyo na Hospitali yetu ya Geita itakuwa ni kipaumbele kwa sababu ina hadhi ya kutosha ili wananchi wa Mkoa wa Geita wapate fursa kubwa ya kupata matibabu katika Mkoa wao.

Name

Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU (K.n.y. JOSEPH K. MUSUKUMA) aliuliza:- Hospitali ya Geita imefanywa kuwa Hospitali ya Mkoa tangu tarehe 8 Januari, 2016:- Je, ni lini DMO aliyekuwa akiongoza Hospitali hiyo atahamia katika hospitali iliyopendekezwa na kikao cha RCC kuwa Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 2

MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona. Nina swali moja dogo tu. Wilaya nyingi mpya za Tanzania hazina Hospitali za Wilaya ikiwemo Wilaya ya Chemba ninakotoka mimi. Je, Serikali itatuhakikishia ndani ya Bunge hili kwamba katika bajeti inayokuja wametenga fedha kujenga hospitali mpya katika Wilaya zote mpya Tanzania?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, ni kweli na naifahamu Chemba, kaka yangu Mheshimiwa Nkamia tumeshaongea sana kufika Chemba pale kuangalia siyo suala zima la afya, lakini na mambo mengine. Ninavyojua ni kwamba katika bajeti ya mwaka huu ambayo tutakuja kuisoma wiki ijayo ina mikakati mbalimbali katika halmashauri mbalmbali. Halmashauri zingine wamejielekeza katika kuboresha vituo vya afya, wengine wamejielekeza katika Hospitali zetu za Wilaya, lakini wengine wamejielekeza katika Hospitali za Mkoa.
Mheshimiwa Spika, katika hili ninavyojua wazi kwamba michakato yote aidha ya ujenzi wa zahanati, Hospitali ya Wilaya au ya Mkoa, vikao husika kwanza vinaanza na mchakato huo. Imani yangu kwamba na wenzetu katika Jimbo la Chemba jambo hilo watakuwa wameliangalia kwa jicho la upana zaidi. Katika haya maana yake Serikali sasa itafanya juhudi kubwa kupeleka resources kutokana na mipango iliyopangwa kutoka katika Halmashauri ili mradi wananchi wetu waweze kupata huduma katika maeneo hayo.