Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 26 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 217 2017-05-16

Name

Susanne Peter Maselle

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUZANA C. MGONUKULIMA (K.n.y. MHE. SUSANE P. MASELLE) aliuliza:-
Je, kwa nini Serikali imewanyang’anya ajira vijana waliokuwa wamejiajiri kwenye Machimbo ya Ishokelahela na baadaye ikaamua kubadili umiliki wa leseni kwa siri?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Susane Peter Maselle, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, wachimbaji wadogo waliokuwa wanachimba Ishokelahela hawakuwa na leseni ya uchimbaji bali walikuwa wanachimba katika eneo la utafiti la leseni ya Kampuni ya Carlton Kitongo Tanzania Limited.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, mwaka 2014, Serikali ilifanya mazungumzo na kampuni hiyo na kuwapatia wachimbaji wadogo hao leseni mbili za uchimbaji zenye jumla ya hekta 20. Wananchi hao waliweza kuunda kampuni yao inaitwa Isinka Federation Miners Co-operative Limited.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2015 kikundi kiliamua kubadilisha leseni zake mbili za uchimbaji mdogo na kuzifanya kuwa leseni moja ya mgodi wa uchimbaji wa kati lakini chini ya Kampuni yao ya Isinka Federation Miners Co-operative Limited. Umiliki wa leseni hizo haujabadilishwa hadi leo upo chini ya umiliki wa wachimbaji hao wadogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi kufikia mwezi Machi, 2017, mgodi ulikuwa umeshakusanya tani 35,000 za mbale (ore) kwa njia ya ubia wa Kampuni ya Busolwa Mining pamoja na wachimbaji hao na waliweza kutoa fursa za ajira 164 za moja kwa moja.