Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUZANA C. MGONUKULIMA (K.n.y. MHE. SUSANE P. MASELLE) aliuliza:- Je, kwa nini Serikali imewanyang’anya ajira vijana waliokuwa wamejiajiri kwenye Machimbo ya Ishokelahela na baadaye ikaamua kubadili umiliki wa leseni kwa siri?

Supplementary Question 1

MHE. SUZANA C. MGONUKULIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nitauliza maswali mawili ya nyongeza kwa niaba ya Mheshimiwa Susane Maselle, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, kutokana na majibu ya Naibu Waziri kuwa wachimbaji hawa wadogo walipata leseni, je, Serikali inatoa kauli gani juu ya Jeshi la Polisi lililotumia nguvu kupiga mabomu wachimbaji hao wadogo na kuwanyanyasa wenyewe na familia zao na kufanyiwa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia wanawake na watoto? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, je, Naibu Waziri yupo tayari kuongozana na Mheshimiwa Susane Maselle kwenda eneo hilo kuongea na wananchi hao kuhusu vitendo walivyofanyiwa na Jeshi la Polisi kuwa hawakufanyiwa kiusahihi kwa sababu walikuwa na leseni? (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na swali la pili, niko tayari kufuatana na Mheshimiwa Susane na kwa ridhaa yako kama itapendeza basi nitafuatana naye, nitembelee maeneo yale. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na wachimbaji hao kupigwa mabomu pamoja na kufanyiwa harassment ni suala ambalo linatakiwa litazamwe kwa kina sana unaweza usiwe na jibu la moja kwa moja. Ninachoweza kusema ni kwamba pale inapotokea kunakuwa na vurugu katika maeneo ya uchimbaji kazi ya Jeshi la Polisi ni kutuliza ghasia ili kuhakikisha kwamba kunakuwa na amani na utulivu katika maeneo yale. Inawezekana ilifanyika katika hatua hiyo, lakini Mheshimiwa Mbunge tutakaa pamoja tuone ni hatua gani zilichukuliwa ili tushirikiane na wenzetu wa Mambo ya Ndani tuone nini cha kufanya zaidi.

Name

Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. SUZANA C. MGONUKULIMA (K.n.y. MHE. SUSANE P. MASELLE) aliuliza:- Je, kwa nini Serikali imewanyang’anya ajira vijana waliokuwa wamejiajiri kwenye Machimbo ya Ishokelahela na baadaye ikaamua kubadili umiliki wa leseni kwa siri?

Supplementary Question 2

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nami nataka niulize swali la nyongeza. Kwa wachimbaji wadogowadogo waliopo katika Mkoa wa Katavi hususan katika Machimbo ya Ibindi na Kapanda, vijana hawa wamekuwa na changamoto kubwa nyingi mno ikiwepo gharama kubwa ya kukata leseni za uchimbaji lakini pia gharama kubwa ya dawa za kusafishia dhahabu wanazopata na gharama za umeme pia ziko juu. Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha sasa inawasaidia hawa vijana kupunguziwa gharama hizi ambazo ni kero? Tamko la Serikali linasema nini ili kuwasaidia vijana kupata mikopo ili wajiendeleze kiuchumi na kupata kipato?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, ni kweli kabisa maeneo ya uchimbaji maarufu sana kwa maeneo ya Mpanda ni pamoja na Ibindi, Kapanda pamoja na Dilifu. Hata hivyo, nimtaarifa Mheshimiwa Mbunge kwamba hatua ambazo Serikali imechukua, la kwanza kabisa ni kurasimisha maeneo hayo ambayo nimeyataja kuwa maeneo maalum kwa ajili ya wachimbaji wadogo na wapo wachimbaji wadogo wazuri sana kwenye eneo lako ikiwa ni pamoja na Mheshimiwa Kapufi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili kuhusu mkakati ambao tunafanya…
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Niseme tu, tumetoa ruzuku mwaka juzi kwa wachimbaji wa Ibindi na Kapanda na bado tunawapatia elimu na uwezeshaji kwa ajili ya uchimbaji mzuri kwa wachimbaji hawa wadogo.

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUZANA C. MGONUKULIMA (K.n.y. MHE. SUSANE P. MASELLE) aliuliza:- Je, kwa nini Serikali imewanyang’anya ajira vijana waliokuwa wamejiajiri kwenye Machimbo ya Ishokelahela na baadaye ikaamua kubadili umiliki wa leseni kwa siri?

Supplementary Question 3

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nami naomba kumuuliza Naibu Waziri swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa kuna migodi ambayo inakuwa imeshafungwa na inakuwa si salama kwa wachimbaji wadogowadogo na hawa wachimbaji wadogowadogo wamekuwa wakikiuka sheria na kuvamia migodi hii na kuhatarisha maisha yao. Je, Serikali ina mikakati gani kuhakikisha uvamizi huu wa wachimbaji wadogowadogo unakwisha na kuchukulia hatua za kisheria?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa, kwa mujibu wa Sheria ya Madini ya 2010, hairuhusiwi kufanya uchimbaji wowote bila leseni na kwa hiyo uvamizi kwa hali ya kawaida hauruhusiwi. Hata hivyo, yapo mazingira ambapo wananchi wamekuwa wakivamia maeneo na hasa ambao wao wameanza kuchimba mapema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu na mkakati wa Serikali, kwanza ni kufanya mazungumzo na hao wachimbaji wadogo kuwaelewesha lakini hata wale wenye leseni ambao wameyashikilia bila kuyaendeleza nao kuzungumza nao. Tunachofanya sasa, maeneo ambayo yanachukuliwa na watafiti bila kuyaendeleza Serikali inayachukua na kuwagawia wachimbaji maalum wadogo kwa utaratibu wa kisheria ili kufanya uchimbaji huu uwe wa manufaa kwa wachimbaji wadogo pamoja na wachimbaji wakubwa.