Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 8 Sitting 4 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 46 2017-09-08

Name

Faida Mohammed Bakar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itatenga bajeti kwa ajili ya kuwajengea nyumba askari polisi wa Pemba ili kuwaondolea adha ya makazi askari hao?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI aliuliza:-
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Faida Mohammed Bakar, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kuwa nyumba za kuishi askari Pemba hazitoshi kama ilivyo katika maeneo mengine nchini na hivyo kusababisha adha kwa askari wetu. Serikali itatenga bajeti katika mwaka ujao wa fedha ili kujenga nyumba za askari wa Zanzibar husasan Pemba ambako Mheshimiwa Mbunge ameuliza ili kuwaondolea adha wanazozipata kutokana na kutokuwa na nyumba za kutosha. (Makofi)