Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 36 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 288 2017-05-29

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RITTA E. KABATI aliuliza:-
Je, ni lini Mahakama zote nchini zitaanza kuendesha kesi kwa lugha ya Kiswahili?

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI NA MICHEZO (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa kifungu cha 12 cha Sheria ya Mahakama Sura ya 11 yaani (Magistrates’ Courts Act CAP 11; S.12), lugha inayotumika kuendesha kesi katika Mahakama zote za Mwanzo ni Kiswahili. Aidha, kifungu hiki kinatamka kwamba kesi katika Mahakama za Wilaya na za Hakimu Mkazi zitaendeshwa kwa Kiswahili ama Kiingereza, isipokuwa hukumu inaandikwa kwa Kiingereza.
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Mahakama Kuu, Kanuni za Lugha za Mahakana ukisoma Kanuni ya (2) inasema kuwa Lugha ya Mahakama Kuu itakuwa Kiswahili au Kiingereza, isipokuwa kumbukumbu za maamuzi, ama hukumu itakuwa kwa lugha ya Kiingereza.
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kanuni za Mahakama ya Rufani ya mwaka 2009, ukisoma Kanuni ya (5) lugha inayotumika katika kuendesha mashauri itakuwa ni Kiswahili au Kiingereza kulingana na maelekezo ya Jaji Mkuu au Jaji anayesikiliza shauri husika, isipokuwa hukumu inaandikwa kwa Kiingereza.
Mheshimiwa Spika, hivyo ninapenda kulihakikishia Bunge lako Tukufu kwamba uendeshaji wa mashauri katika Mahakama zote nchini kwa mujibu wa Sheria na Kanuni zilizopo unaruhusu kutumia lugha zote mbili, Kiswahili na Kiingereza na tumekuwa tukizingatia lugha hizo katika uendeshaji wa mashauri.