Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 02 2017-11-07

Name

Amina Nassoro Makilagi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE (K.n.y. MHE. AMINA N. MAKILAGI) Aliuliza:-
Wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma katika Kata za Etaro, Ifulifu, Nyegina na Nyakatende wanakabiliwa na taizo la maji.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia wananchi wa kata hizo maji safi na salama?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kabla sijajibu swali la Mheshimiwa Amina Makilagi naomba kwanza nitoe shukrani zangu za dhati kwa Mheshimiwa Rais kwa imani kubwa aliyoionyesha kwangu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais , TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Amina Nassor Makilagi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma katika Kata za Itaro, Ifulifu, Nyegina na Nyakatende wanakabiliwa na tatizo la maji kwa sababu mahitaji halisi ya maji katika kata hizo ni lita 953,550 wakati uzalishaji wa maji katika vyanzo vilivyopo ambavyo ni visima sita katika Vijiji vya Keimba na Kabegi kwenye Kata ya Ifulifu, Kijiji cha Mkikira katika Kata ya Nyegina na Vijiji vya Kigera, Nyegina na Kamguruki katika Kata ya Nyakatende vinazalisha lita 5,100 kwa siku pamoja na mradi wa maji ya bomba katika Kata ya Nyegina unazalisha lita 50,000 kwa siku na hivyo kufanya jumla ya lita zinazozalishwa kwa sasa kuwa 55,100 tu ambazo ni asilimia sita ya mahitaji.
Mheshimiwa Spika, katika juhudi za kuboresha huduma za maji kwenye eneo hilo, Serikali inakamilisha ujenzi wa mradi mkubwa wa maji utakaohudumia wakazi wa Manispaa ya Musoma pamoja na wakati wa Kata za Nyamkanga, Bukabwa na Busimwa katika halmashauri ya Wilaya ya Butiama na wakazi kwenye Kata za Etaro, Nyegina na Nyakatende katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Hadi sasa Serikali imeshapeleka shilingi milioni 900 kwenye Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Musoma, ambayo inasimamia utekelezaji wa mradi huo.
Mheshimiwa Spika, kazi ambazo zimeshatekelezwa hadi sasa ni kupima njia ya bomba, kuchonga barabara kuelekea Mlima Balima kutakakojengwa tenki lenye ujazo wa lita milioni mbili ambalo litasambaza maji kwa mtiririko kupeleka huduma za maji safi na salama katika kata nilizotaja. Aidha, taratibu za ununuzi wa mabomba yenye urefu wa kilometa 35 zimekamilika.