Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 26 2017-11-08

Name

Jaku Hashim Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. JAKU HASHIM AYOUB aliuliza:-
Tarehe 25/5/2017 Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi akijibu swali Na. 274 kuhusu madai ya mkandarasi aliyejenga vituo vya polisi Mkokotoni Unguja na Madungu alisema, deni tayari limeshahakikiwa na kwamba atalipwa mara fedha zitakapotolewa lakini huu ni mwaka wa tano deni hilo halijalipwa:-
(a) Je, Serikali ina nia thabiti ya kumlipa mkandarasi?
(b) Je, Serikali inasubiri ipelekwe Mahakamani ndipo ilipe deni hilo?
(c) Je, huu ndiyo utawala bora ambao nchi yetu ina dhamira ya kuujenga?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jaku Hashim Ayoub, Mbunge wa Baraza la Wawakilishi, lenye sehemu (a), (b), na (c) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua madeni ya wakandarasi wote akiwemo Albatna Building Contractor na ina nia ya dhati ya kuyalipa madeni yote ya wakandarasi na Washauri Elekezi waliohusika katika miradi mbalimbali ikiwemo miradi iliyohusisha Jeshi la Polisi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2017/2018, Jeshi la Polisi limetenga jumla ya shilingi bilioni 2.2 kwa ajili ya kupunguza madeni ya wakandarasi waliotekeleza miradi mbalimbali ikiwemo mradi wa ujenzi wa Kituo cha Polisi Mkokotoni ambao umetengewa jumla ya shilingi milioni 200 ikiwa ni sehemu ya deni ambalo anadai mkandarasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nilihakikishie Bunge lako Tukufu kuwa hakuna deni la mzabuni au mtumishi ambalo halitalipwa kwani madeni yote yaliyohakikiwa yanaendelea kulipwa kwa kadri fedha zitakavyokuwa zinapatikana.