Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 52 2016-04-27

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza:-
Je, Serikali kupitia REA inachukua hatua gani kwa Mkandarasi CHICCO ambaye ameshindwa kukamilisha utekelezaji wa Mradi wa Kupeleka Umeme Vijijini Awamu ya Pili (REA II) katika vijiji vya Mwangoye, Mbutu na Mambali?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Selemani Jumanne Zedi, Mbunge wa Bukene, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Mkandarasi CHICCO kutoka China alishinda zabuni ya usambazaji wa umeme vijijini REA Awamu ya Pili katika Mkoa wa Tabora. Ni kweli kwamba mkandarasi huyu alianza kazi kwa kusuasua hali iliyosababisha Wakala wa Nishati Vijijini kuchukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kumwandikia barua ya kutoridhishwa na kazi na kuongeza usimamizi wa kufuatilia utendaji wake. Hatua nyingine iliyochukuliwa ni pamoja na kumtaka mkandarasi huyo kuongeza kampuni nyingine (sub-contractor) ili kuharakisha shughuli za ujenzi wa mradi huo. Utekelezaji wa kazi hiyo wa mkoa mzima unaendelea ambapo kazi imekamilika kwa asilimia 82 na mradi unatarajiwa kukamilika mwishoni wa mwezi Juni, 2016.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya kupeleka umeme vijiji vya Mambali, Mbutu pamoja na Mwangoye inaendelea na imefikia utekelezaji kama ifuatavyo:-
(i) Kijiji cha Mambali kazi ya kupeleka umeme imekamilika kwa asilimia 100 na wateja wapatao 49 wameunganishiwa umeme.
(ii) Kijiji cha Mwangoye kazi ya kujenga njia ya umeme imekamilika. Taratibu za ufungaji wa transfoma zinaendelea na umeme unatarajiwa kuwashwa mara baada ya kukamilika kwa ufungaji wa transfoma hizo.
(iii) Kijiji cha Mbutu hakikuwepo kwenye mradi huu hata hivyo mkandarasi CHICCO alipewa kazi ya ziada na mradi unaendelea. Mkandarasi amemaliza kazi ya upembuzi yakinifu na sasa yupo katika hatua za mwisho za kukamilisha michoro ya kiuhandishi kabla ya kuanza utekelezaji wa mradi wa umeme katika kijiji hiki.