Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 9 Sitting 7 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 93 2017-11-15

Name

Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SILAFU J. MAUFI
Serikali imerejesha mafunzo ya JKT nchini. Je, ni lini Kambi ya JKT ya Luwa Mkoani Rukwa itafufuliwa ili kuandaa vijana wetu?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI (K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Silafu Maufi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kambi ya Luwa JKT ilifufukiwa na sasa kimekuwa Kikosi na kimepewa namba 846 Kikosi cha Jeshi yaani 846 KJ kuanzia tarehe 01 Desemba, 2016.
Aidha, vikosi vilivyoanzishwa sambamba na kikosi hicho ni pamoja na Kikosi cha Jeshi 826 kilichopo Mpwapwa hapa Dodoma, 839 Kikosi cha Jeshi kilichopo Makuyuni, Mjini Arusha, 845 Kikosi cha Jeshi kilichopo Itaka, Mkoani Songwe na 847 Kikosi cha Jesi kilichopo Milundikwa, Mkoani Rukwa.