Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SILAFU J. MAUFI Serikali imerejesha mafunzo ya JKT nchini. Je, ni lini Kambi ya JKT ya Luwa Mkoani Rukwa itafufuliwa ili kuandaa vijana wetu?

Supplementary Question 1

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninashukuru hayo majibu niliyopewa na Mheshimiwa Waziri, lakini niliuliza swali kwamba kufufuliwa Kambi ya JKT, sikuuliza swali la kwamba mabadiliko ya matumizi ya Kambi ya JKT, la hasha. Sasa nina maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa tunajua wazi kwamba kujiunga kwa vijana wetu kwenye JKT ndiko ambako kuna chachu ya kuwawezesha wao kujiunga na Polisi, kujiunga na JWTZ na kadhalika. Sasa je, ni sababu zipi zilizopelekea kutoka JKT na kuwa Kikosi cha Jeshi na kusababisha Mkoa wetu wa Rukwa kukosa Kambi ya Jeshi?
Swali la pili, je, vijana wetu ambao wanauhitaji wa kujiunga na JKT wa Mkoa wa Rukwa kutokana na wingi wao wa kila mwaka kuongezeka ndani ya jamii, je, hawa vijana watanufaika vipi na vikosi hivyo ambavyo vimebadilishwa makambi yao kuwa ni vikosi vya Jeshi au watajengewa Kambi ya Jeshi upande gani? Naomba uniambie katika Mkoa wetu wa Rukwa. (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI (K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mbunge kwa kuguswa kwake na vijana hasa hasa wa Mkoa wa Rukwa na hoja yake ya kutaka vijana wapate fursa hiyo, lakini nimhakikishie tu ninapojibu maswali yake yote mawili kwa pamoja ni kwamba Kambi la Jeshi kubwa hasa linaloangaliwa ni suala la kibajeti.
Natambua katika nchi nzima vijana wengi hata maeneo ambako kuna Kambi wengi sana wanajitokeza kuomba nafasi hizo, unaweza ukakuta Wilaya ambako wamejitokeza vijana kama 500, idadi inayotakiwa kupatikana labda ni 50 mpaka 60 kwa maana hiyo sisi kama Serikali tunapokea tu hoja ya Mbunge na uhitaji mkubwa huo wa kuona vijana wanataka kujitolea kwenda kujenga Taifa ili tuliangalie kwenye upande wa bajeti kwasababu kwenye upande wa makambi hilo ni jambo rahisi tu ambalo wanaweza wakakaa tu katika Kambi yoyote ile na mafunzo haya yakaendelea kama ambavyo inafanyika katika mikoa mingine.