Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 58 2016-04-27

Name

Musa Rashid Ntimizi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. MUSA R. NTIMIZI aliuliza:-
Wananchi wa Kata ya Loya katika Halmashauri ya Tabora (Uyui) wameitikia wito wa Serikali wa ulinzi kwa kujenga kituo kikubwa cha polisi katika kata yao:-
(a) Je, ni lini kituo hicho kitafunguliwa hasa ikizingatiwa kuwa Loya ni zaidi ya kilometa 120 kutoka Makao Mkuu ya Wilaya Isikizya ambako ndiko kwenye kituo cha polisi?
(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaongezea bajeti ya mafuta ili kuwarahisishia watendaji kazi maana maeneo ya Jimbo ni kubwa na yote yanahitaji huduma za kipolisi?

Name

Charles Muhangwa Kitwanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

WAZIRI MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Musa Rashid Ntimizi, Mbunge wa Igalula, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kwanza kuwashukuru wananchi na wadau wote walihusika katika kuchangia ujenzi wa Kituo cha Polisi Kata ya Loya katika Halmashauri ya Tabora (Uyui). Pamoja na mwitikio huo bado kituo hiki hakijakamilika sehemu ya kuhifadhia silaha, huduma ya choo na makazi ya askari. Pindi vitu hivi vitakapokamilika kituo hiki kitafunguliwa na askari watapelekwa. Hivyo basi, namuomba Mheshimiwa Mbunge kuendelea na jitihada za kuwahamasisha wananchi wa Kata ya Loya ili kukamilisha ujenzi huo.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina mpango wa kuongeza bajeti ya mafuta katika maeneo mbalimbali kulingana na upatikanaji wa fedha ili kukidhi mahitaji ya doria, misako na operesheni mbalimbali katika kutoa huduma ya ulinzi na usalama kwa wananchi.