Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 9 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 114 2018-02-09

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENAN (k.n.y MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA) aliuliza
(a) Je, kuna sheria yoyote ya nchi inayomruhusu askari polisi kumkatamata mtuhumiwa, kumpiga na kumtesa kabla hajajua kosa lake na kabla ya kufikishwa katika Kituo cha Polisi?
(b) Je, Serikali inachukua hatua zipi za kuhakikisha kuwa askari wanaofanya vitendo kama hivyo wanawajibishwa kwa mujibu wa sheria za nchi?
(c) Je, mpaka sasa ni askari wangapi wameshachukuliwa hatua za kisheria kutokana na makosa ya kujichukulia hatua mkononi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum lenye shemu (a),(b) na (c) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Sura ya 20 kifungu cha 11 kinaeleza namna ya ukamataji. Aidha, kifungu hiki mahsusi cha ukamataji hakimruhusu askari kumpiga na kumtesa raia wakati wowote anapokuwa kizuizini.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Kanuni za Utendaji wa Jeshi la Polisi (PGO) askari yoyote anapobainika kufanya vitendo vya kupiga au kutesa raia huchukuliwa hatua za kinidhamu ikiwemo kufukuzwa kazi na au hata kufikishwa mahakamani.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha januari mpaka Desemba, 2017 jumla ya askari 105 waliotenda makosa mbalimbali walichukuliwa hatua za kinidhamu ikiwa ni pamoja na kufukuzwa kazi.