Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 2 Education, Science,Technology and Vocational Training, Ofisi ya Rais TAMISEMI. 16 2016-01-27

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY aliuliza:-
Nyumba za kuishi walimu ni chache katika maeneo yao ya kazi na
mishahara yao pia ni midogo kuweza kumudu upangaji wa nyumba mitaani.
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba za walimu na
kuboresha mishahara yao?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kiswaga Boniventura Destery, Mbunge wa Magu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, mahitaji ya nyumba za walimu wa Shule za Msingi katika Halmashauri ya Magu ni 1,447, zilizopo ni nyumba 284 na upungufu ni nyumba 1,183. Aidha, Shule za Sekondari zina mahitaji ya nyumba 396, zilizopo ni nyumba 53 na upungufu ni nyumba 343.
Mheshimiwa Spika, kupitia Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari ya Awamu ya Pili (MMES II), Halmashauri imepokea shilingi milioni 326.8 ambazo zitatumika kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya nyumba za walimu. Kwa upande wa Shule za Msingi, Serikali katika mwaka wa fedha 2015/2016 imetenga shilingi milioni 100 kutokana na mapato ya ndani kwa ajili ya ujenzi wa nyumba tano na shilingi milioni 127 zimetengwa kupitia ruzuku ya maendeleo (CDG) kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa nyumba sita za walimu.
Mheshimiwa Spika, kuhusu kuboresha mishahara ya walimu, Serikali imekuwa ikitoa nyongeza za mishahara kila mwaka kadiri uchumi unavyoruhusu. Kwa mfano, mwaka 2007/2008 hadi mwaka 2015/2016 mshahara wa mwalimu mwenye cheti yaani astashahada, uliongezeka kwa asilimia 156.28 kutoka shilingi 163,490/= hadi shilingi 419,000/= kwa mwezi. Mshahara wa mwalimu mwenye stashahada uliongezeka kwa asilimia 160.2 kutoka shilingi 203,690/= hadi shilingi 500,030/=; na kwa mwalimu mwenye shahada kwa asilimia 121.05 kutoka shilingi 323,900/= hadi shilingi 716,000/= kwa mwezi. Serikali imekuwa ikiboresha mishahara hiyo kwa kuzingatia umuhimu wa kazi wanayofanya walimu. Hata hivyo, Serikali inaendelea kuboresha mishahara ya walimu na watumishi wengine kwa kadiri hali ya kifedha inavyoruhusu.