Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY aliuliza:- Nyumba za kuishi walimu ni chache katika maeneo yao ya kazi na mishahara yao pia ni midogo kuweza kumudu upangaji wa nyumba mitaani. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba za walimu na kuboresha mishahara yao?

Supplementary Question 1

MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini naomba niulize maswali madogo mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa Serikali imekiri kuwa kuna upungufu wa nyumba 1,183 za kuishi walimu na sasa tayari wananchi wa Wilaya ya Magu wameshajenga maboma 27 yapo tayari kukamilishwa; je, Serikali inaweza kutusadia fedha za kukamilisha ili walimu waingie kwenye nyumba hizo kupunguza uhaba wa nyumba za walimu?
Swali la pili, kwa kuwa nyumba hazitoshi, je, Serikali inaonaje kuwasaidia walimu ambao wanapanga nje mitaani kuwaongeza mishahara kidogo ili waweze kumudu upangaji wa nyumba mitaani? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA) Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza napenda kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa juhudi hii kubwa anayoifanya katika Jimbo lake na kwa sababu wamejenga maboma 27, hii inaonyesha ni commitment, jinsi gani watu wa Magu wameendelea kujitahidi kuhakikisha kwamba Walimu wanapata fursa ya kuishi katika nyumba bora.
Mheshimiwa Spika, kwa sababu request imesema ni jinsi gani Serikali itaweza ku-top up hiyo amount? Nasema, ni lazima tuangalie, tufanye ile resource mobilization kutoka katika pande zote.
Mheshimiwa Spika, napenda kumshauri Mheshimiwa Mbunge kwamba katika allocation ya own sources katika Halmashauri zetu, tuangalie ni jinsi gani tutafanya kupitia vyanzo mbalimbali katika Halmashauri; na bahati nzuri sasa hivi tumefanya uboreshaji mkubwa sana katika ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri zetu. Nakiri kwamba Halmashauri zimefanya kazi kubwa sana baada ya kuwapa commitment wahakikishe wanakusanya own source kwa kutumia electronic devices na hili wamelifanya.
Mheshimiwa Spika, nina mategemeo makubwa sana kwamba Halmashauri ya Magu hivi sasa, maana yake mapato yake yataongezeka kwa kasi. Naomba nimwambie kwamba Serikali kupitia TAMISEMI, itashirikiana na Halmashauri ya Magu kuona jinsi gani tutayafanya mpaka maboma hayo yaweze kukamlika. Lengo ni kwamba walimu wetu waishi katika mazingira salama na wapate motisha ya kufundisha.
Mheshimiwa Spika, katika sehemu (b) ya swali lake linasema, jinsi gani kama kutakuwa na topping allowance ilimradi walimu waweze kupata jinsi gani watakapokuwa mitaani waweze kulipia lile suala la pango.
Mheshimiwa Spika, naomba nikiri kwamba ni kweli tuna wafanyakazi mbalimbali ambao wanaishi katika mazingira magumu; acha walimu, acha sekta ya afya, acha mabwana shamba, wote wapo katika mazingira mbalimbali. Hili Serikali imeliona, ndiyo maana katika jibu langu la msingi mwanzo nilisema kwamba lazima tuhakikishe kwamba mishahara inaboreshwa ili mwisho wa siku hata mwalimu akikaa mtaani aweze kuwa na ile purchasing power ya kulipia nyumba. Ahsante.
SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na swali linalofuata. Tuko Wizara hiyo hiyo ya TAMISEMI; swali la Mheshimiwa Omary Tebweta Mgumba, Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki.