Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 49 Energy and Minerals Wizara ya Madini 404 2017-06-16

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza:-
Katika maeneo ya Bugarama, Wilaya Ngara kuna Mgodi wa Kabanga Nickel uliodumu kwa miaka 30 sasa na kampuni mbalimbali zimekuwa zikiendesha shughuli zake kwenye mgodi huo na kuondoka tangu mwaka 1970 wakidai kuwa wanafanya utafiti huku bei ya Nickel katika soko la dunia akishuka.
Je, wananchi wa Ngara hususan maeneo ya Bugarama watanufaika na uwepo wa rasilimali hiyo iliyopo kwenye maeneo hayo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Oliver Daniel Semuguruka, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kampuni ya Kabanga Nickel inamiliki mradi wa utafutaji madini ya Nickel katika eneo la Kabanga chini ya leseni namba moja ya mwaka 2009 iliyotolewa tarehe 02 Mei, 2009. Kampuni hiyo inaendelea kufanya utafiti wa kina ili kubaini kama mradi huo unaweza kuendelezwa kwa faida zaidi. Hivi karibuni bei ya madini ya Nickel ilishuka ghafla kutoka dola za Marekani 11 kwa pound mwaka 2010 hadi dola za Marekani 4 kwa pound kwa mwaka 2014. Kutokana na hali hiyo, kampuni inatarajia kuendeleza shughuli za uchimbaji mara baada ya bei hiyo kuimarika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi tarehe 4 Aprili, 2017 bado bei ya Nickel katika soko la Dunia ilikuwa dola 4.45 kwa pound ikilinganishwa na bei ya dola 11 mwaka 2009 mradi ulipokuwa ukifanyiwa upembuzi yakinifu. Mgodi unatarajiwa kutoa ajira 1,455 wakati ujenzi ukiendelea na wakati wa uzalishaji itaajiri Watanzania 800. Mradi utakapoanza kupata faida mambo yatakayofanya wananchi wanufaike ni pamoja na kulipa service levy, kutoa huduma za Maendeleo pamoja na ajira hapa nchini. Kadhalika tutajenga miundombinu kwa ajili ya kusaidia jamii.