Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza:- Katika maeneo ya Bugarama, Wilaya Ngara kuna Mgodi wa Kabanga Nickel uliodumu kwa miaka 30 sasa na kampuni mbalimbali zimekuwa zikiendesha shughuli zake kwenye mgodi huo na kuondoka tangu mwaka 1970 wakidai kuwa wanafanya utafiti huku bei ya Nickel katika soko la dunia akishuka. Je, wananchi wa Ngara hususan maeneo ya Bugarama watanufaika na uwepo wa rasilimali hiyo iliyopo kwenye maeneo hayo?

Supplementary Question 1

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina masawali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mgodi wa Kabanga Nickel una mda mrefu sana, kama nilivyouliza kwenye swali langu la msingi, tangu mwaka 1970 na wachimbaji walianza tangu mwaka 1973. Wananchi wa Ngara tulikuwa tukiona ndege za wazungu zikija na kuondoka wakidai kwamba wanapeleka sample na hawarudi tena, isije ikawa kama makinikia. Je, huu mgodi wa Kabanga Nickel utaanza lini rasmi ili wananchi wa Ngara na Serikali kwa ujumla tuweze kunufaika? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; Sheria na mauziano ya Makampuni inataka mnunuzi na muuzaji kulipa kodi ya Serikali. Mgodi wa Kabanga Nickel umekwisha kubadilisha wamiliki zaidi ya wanne. Je, Serikali Kuu na Halmashauri Kuu ya Wilaya ya Ngara imenufaika vipi na huo umiliki wa kubadilisha wamiliki kila mara?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa Semguruka kwa jinsi anavyofuatilia maslahi ya wananchi wa Mkoa wa Kagera pamoja na wananchi wa Ngara kwa ujumla wake. Nampongeza pia anavyoshirikiana na Waheshimiwa Wabunge wengine majirani wa Biharamulo, Ngara na wengine, hongera sana Mheshimiwa Semuguruka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na swali la kwanza. Ni kweli kabisa huu mradi umeanza tangu mwaka 2009, kwa kweli si miaka ya 1970 iliyopita. Hata hivyo niseme tu kwamba kazi inayofanyika sasa hivi ni kukamilisha upembuzi yakinifu, na natarajia kufungua mgodi mara tu baada ya bei ya nickel kuimarika. Hata hivyo tumempa muda wa mwaka asipofanya hivyo eneo hilo tutalichukua tutawamilikisha wawekezaji wengine wenye nia na uwezo wa kufanya kazi hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, manufaa yatakayopatikana mgodi huo ukifunguliwa ni pamoja na kutoa ajira kwa wananchi wengi wa Bugarama na Kanyenyi, kadhalika watalipa mafao ya Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusiana na uhamishaji, Sheria za Kodi zinamtaka mmiliki yeyote akihamisha au kuuza hisa au leseni yake anatakiwa kulipa capital gain ya asilimia 10 na kwa upande wa Sheria ya Madini kifungu cha 9(1) cha mwaka 2010 kinataka mmiliki akianza kuhamisha analipa dola 3,000. Kwa hiyo, atakapofika hatua hiyo Mheshimiwa Semuguruka haya mafao ya Serikali yataingia. (Makofi)

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza:- Katika maeneo ya Bugarama, Wilaya Ngara kuna Mgodi wa Kabanga Nickel uliodumu kwa miaka 30 sasa na kampuni mbalimbali zimekuwa zikiendesha shughuli zake kwenye mgodi huo na kuondoka tangu mwaka 1970 wakidai kuwa wanafanya utafiti huku bei ya Nickel katika soko la dunia akishuka. Je, wananchi wa Ngara hususan maeneo ya Bugarama watanufaika na uwepo wa rasilimali hiyo iliyopo kwenye maeneo hayo?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira kule Mbeya umekuwa static kwa muda mrefu sana na Mgodi huu mimi naweza nikasema sasa wananchi wa Mkoa wa Mbeya na mikoa ya jirani tumekuwa yatima. Nini tamko la Serikali, nashukuru. (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana nae kwanza Mwanjelwa hongera sana. Hata mwaka jana amehangaika sana kuhakikisha kwamba mgodi huu unafanya kazi. Nimpe taarifa tu, mwaka 2017/2018 Shirika la STAMICO limeanza uchimbaji, na hivi sasa limeishachimba tani 500 ya makaa ya mawe na wataendelea na uchimbaji. Kadhalika kuna makampuni mawili yataingia ubia ili kuwezesha uchimbaji kuwa wa manufaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mgodi wa Kiwira umeishaanza shughuli na kufika mwaka 2018/2019 tunatarajia tani 100,000 zitakuwa zimezalishwa katika mgodi ule. (Makofi)

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza:- Katika maeneo ya Bugarama, Wilaya Ngara kuna Mgodi wa Kabanga Nickel uliodumu kwa miaka 30 sasa na kampuni mbalimbali zimekuwa zikiendesha shughuli zake kwenye mgodi huo na kuondoka tangu mwaka 1970 wakidai kuwa wanafanya utafiti huku bei ya Nickel katika soko la dunia akishuka. Je, wananchi wa Ngara hususan maeneo ya Bugarama watanufaika na uwepo wa rasilimali hiyo iliyopo kwenye maeneo hayo?

Supplementary Question 3

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana nashukuru. Katika milima ya Panda Hill Wilaya ya Mbeya kuna madini ya niobium ambayo yanatarajiwa kuchimbwa hivi karibuni. Je, Serikali imechukua hatua gani na tahadhari gani ili yasije yakatokea yale yaliyotokea kwenye Acacia na Barrick Gold Cooperation?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru sana, Mgodi wa Niobium hapa Tanzania ni mgodi pekee ambao unapatikana katika eneo la Songwe. Kinachofanyika sasa ni majadiliano kati ya Magereza ambako eneo la mgodi litachukua ili kuona kama kutakuwa na re-settlement na majadiliano kama yakikamilika.
Kwa hiyo, nimpe taarifa tu, taratibu zinazofanyika sasa ni majadiliano kati ya Kampuni pamoja na Magereza, taratibu zikishakamilika basi uwekezaji utaendelea.

Name

Tundu Antiphas Mughwai Lissu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza:- Katika maeneo ya Bugarama, Wilaya Ngara kuna Mgodi wa Kabanga Nickel uliodumu kwa miaka 30 sasa na kampuni mbalimbali zimekuwa zikiendesha shughuli zake kwenye mgodi huo na kuondoka tangu mwaka 1970 wakidai kuwa wanafanya utafiti huku bei ya Nickel katika soko la dunia akishuka. Je, wananchi wa Ngara hususan maeneo ya Bugarama watanufaika na uwepo wa rasilimali hiyo iliyopo kwenye maeneo hayo?

Supplementary Question 4

MHE. TUNDU A. M. LISSU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri kuhusiana na huo mgodi unaopangwa kujengwa wa Kabanga Nickel, Serikali itapata asilimia ngapi kama mrahaba kwa mujibu wa Sheria za Tanzania? (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Tundu Lissu, Mbunge mashuhuri kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimueleza Mheshimiwa Tundu Lissu; Mrabaha unaotozwa kwa sasa kwa mujibu wa Sheria ya Madini ya mwaka 2010 madini yote ya ujenzi ikiwa pamoja na madini ya chumu na iron ambayo ni nickel ni asilimia tatu, lakini madini mengine ya dhahabu ni asilimia nne na madini mengine ni asilimia moja, madini ya almasi ni asilimia tano. Kwa hiyo, asilimia tutakazopata kutoka kwenye mgodi ni pamoja na hiyo. (Makofi)