Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 57 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 474 2017-06-30

Name

Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DANIEL E. MTUKA aliuliza:-
Taarifa ya Idara ya Upimaji wa Ramani ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi inalitaja eneo la Chisinjisa lililopo Wilaya ya Manyoni kuwa ndipo alama pekee ya katikati (center point) ya Tanzania inapatikana.
• Je, ni lini Serikali italitambua rasmi eneo hili na kulitangaza katika Gazeti la Serikali?
• Je, Serikali haioni umuhimu wa kuendeleza na kulitangaza eneo hili ili kuvutia utalii wa ndani na nje kama chanzo cha mapato?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARIDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi naomba kujibu swali namba 474 kutoka kwa Mheshimiwa Daniel Edward Mtuka, Mbunge wa Manyoni Mashariki, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, hakuna taarifa rasmi za kitaalam zilizobainisha kwamba Kijiji cha Chisinjisa ndipo alama pekee ya katikati (center point) ya Tanzania pamoja na wenyeji wa eneo hilo kudai kuwepo kwa alama hiyo eneo la Sukamahela.
Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kupitia Idara ya Upimaji na Ramani inakusudia kufanya utafiti wa kina kwa kutumia elimu ya jiometriki (geometics) ili kubaini eneo rasmi ambalo alama ya katikati (center point) ya Tanzania inapatikana.
Mheshimiwa Spika, baada ya utafiti huo kukamilika eneo la katikati ya Tanzania litatangazwa katika Gazeti la Serikali. Aidha, mamlaka zinazohusika na masuala ya utalii zitaliendeleza eneo husika ilikuvutia utalii wa ndani na nje kama zinavyofanya nchi nyingine duniani na kuongeza mapato ya Serikali.