Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 20 2018-04-05

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:-
Barabara ya kutoka Mima hadi Mkanana ni mbaya sana na inapitika kwa shida sana wakati wote; na Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa haina uwezo kifedha wa kuifanyia mategenezo makubwa:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuifanyia matengenezo makubwa barabara hiyo ili iweze kupitika wakati wote?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa George Malima Lubeleje, Mbunge wa Mpwapwa, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Mima hadi Mkanana ni barabara mlisho ya tabaka la udongo yenye urefu wa kilometa 26.5, inayounganisha barabara ya Kibakwe hadi Wotta yenye urefu wa kilometa 26 na barabara ya Gulwe hadi Seluka yenye urefu wa kilometa 64.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kuifanyia matengenezo barabara hiyo ili kuboresha huduma za usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa Vijiji vya Mima na Mkanana. Katika mwaka wa fedha 2016/2017 shilingi milioni 40.84 zilitumika kufanyia matengenezo ya sehemu korofi urefu wa kilometa nne.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mpango wa bajeti wa mwaka wa fedha 2018/2019, TARURA imetenga shilingi milioni 57 kwa ajili ya matengenezo ya sehemu korofi urefu wa kilometa 6.5 na matengenezo ya kawaida urefu wa kilometa 10 ili iweze kupitika kwa wakati wote.