Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:- Barabara ya kutoka Mima hadi Mkanana ni mbaya sana na inapitika kwa shida sana wakati wote; na Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa haina uwezo kifedha wa kuifanyia mategenezo makubwa:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuifanyia matengenezo makubwa barabara hiyo ili iweze kupitika wakati wote?

Supplementary Question 1

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, tarehe 30 Desemba, 2017, Waziri wa TAMISEMI, Mheshimiwa Jafo alitembelea Kijiji cha Mima na kuona barabara ya Mima ilivyo mbaya na nilimwonyesha ni barabara ya kwenda Mkanana, ile barabara kilometa 26 zote ni mawe matupu wala hakuna udongo kule, yote ni mbaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa Mheshimiwa Naibu Waziri anaposema anatengeneza eneo korofi, hili eneo lote kubwa linalobaki atatengeneza nani na wananchi wa Mkanana, Kibwegele wana shida? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Mheshimiwa Waziri alipotembelea Mpwapwa tarehe 30 Desemba alikakuga barabara ya lami kilometa moja Mjini Mpwapwa na aliwaahidi wananchi wa Mji wa Mpwapwa kwamba kilometa zote 10 watazijenga kwa kiwango cha lami. Mbona sijaiona bajeti hii ya kujenga barabara za lami Mpwapwa Mjini kilometa 10? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Lubeleje, senior MP, ambaye mimi huwa napenda kumuita greda la zamani makali yaleyale kutokana na kazi yake kubwa anayoifanya kule Mpwapwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nikiri wazi kwamba nilikuwa na Mheshimiwa Lubeleje katika Jimbo lake na ni kweli barabara ile ina changamoto kubwa na hata siku ile tulivyoenda kukagua kituo cha afya cha Mima tulitumia muda mrefu sana kutokana na changamoto za barabara ile. Hata hivyo, niliwaagiza wataalam kwamba wafanye uchambuzi wa kutosha nini kifanyike katika barabara ile, maana ukiangalia wigo wake, siyo hiyo peke yake, barabara hizo zote ambazo anazizungumzia Mzee Lubeleje ziko katika hali mbaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, japokuwa bajeti iliyokuwepo hapa ni ndogo lakini kupitia Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) tunaziweka katika mpango wa utekelezaji maalum kwa kuzitafutia fedha kwa sababu eneo lile lina changamoto kubwa. Kwa hiyo, naomba nimwombe Mheshimiwa Lubeleje avute subira kwani ofisi yetu inafanya kazi kwa sababu wataalam nimewatuma kufuatilia kazi ile.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu barabara za Mji wa Mpwapwa, ni kweli, mpango uliokuwepo pale ni takribani kilometa tano lakini mtandao wote wa barabara ya lami ni karibu kilometa 10 Mjini Mpwapwa. Hivi sasa wakandarasi wanaendelea na kazi na katika mpango wa bajeti ya mwaka huu, majibu ya Naibu Waziri alipokuwa anazungumza hapa ambayo ni mazuri sana yalikuwa yakijibu suala zima la Mtanana lakini suala la mtandao wa barabara za lami katika mpango wa bajeti ya mwaka huu Mheshimiwa Lubeleje ataona jinsi gani Serikali imejipanga kutekeleza mpango ule wala asiwe na hofu.

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:- Barabara ya kutoka Mima hadi Mkanana ni mbaya sana na inapitika kwa shida sana wakati wote; na Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa haina uwezo kifedha wa kuifanyia mategenezo makubwa:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuifanyia matengenezo makubwa barabara hiyo ili iweze kupitika wakati wote?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Mvua zinazoendelea zimeharibu barabara nyingi sana za vijijini karibu nchi nzima mfano katika Jimbo langu la Rombo barabara nyingi sana za vijijini hazipitiki. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, natambua TARURA inafanya kazi nzuri sana sasa hivi katika baadhi ya majimbo. Natambua pia kwamba kuna bajeti itasomwa hapa kwa ajili ya kuiwezesha TARURA kuendelea na kazi zake. Je, Serikali ina mpango wowote wa dharura wa kuisaidia TARURA ili iweze kuwezesha barabara ambazo zimevunjika vijijini kupitika kwa sasa hivi ili wananchi waweze kupeleka mazao yao katika masoko na kadhalika? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli mvua zimenyesha kubwa katika maeneo mengi na kila neema inavyokuja huwa inakuwa na adha yake. Ni wajibu wetu kuhakikisha kwamba barabara zote zinapitika kwa vipindi vyote. Ni vizuri tukapata fursa ya kufanya uthamini maeneo ambao yameharibiwa na mvua ili hatua za dharura ziweze kuchukuliwa na wananchi wetu wasiweze kuendelea kupata shida.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:- Barabara ya kutoka Mima hadi Mkanana ni mbaya sana na inapitika kwa shida sana wakati wote; na Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa haina uwezo kifedha wa kuifanyia mategenezo makubwa:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuifanyia matengenezo makubwa barabara hiyo ili iweze kupitika wakati wote?

Supplementary Question 3

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii nami niulize swali dogo la nyongeza. Kuna ahadi nyingi tuliwaahidi wananchi wetu wakati tukiomba kura ikiwemo Mheshimiwa Rais kuahidi wananchi wa Itigi kuwajengea barabara ya lami inayoingia katika Mji wa Itigi kilometa nane. Je, ni lini sasa Wizara hii itatekeleza ahadi hii?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna ahadi nyingi ambazo zilitolewa wakati wa kampeni na yeye mwenyewe Mheshimiwa Mbunge alitoa ahadi zake na Mheshimiwa Rais alitoa ahadi katika maeneo ambayo alienda kuomba kura. Katika kipindi ambacho aliomba na kutoa ahari ahadi utekelezaji wake ni ndani ya miaka mitano. Upo utaratibu ambao umewekwa mahsusi ili kuhakikisha kwamba ahadi zote ambazo zilitolewa na Mheshimiwa Rais zitaenda kutekelezwa. Naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira, Ilani ya CCM inatekelezwa ndani ya miaka mitano na sisi ni waungwana tukiahidi huwa tunatekeleza.

Name

Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:- Barabara ya kutoka Mima hadi Mkanana ni mbaya sana na inapitika kwa shida sana wakati wote; na Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa haina uwezo kifedha wa kuifanyia mategenezo makubwa:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuifanyia matengenezo makubwa barabara hiyo ili iweze kupitika wakati wote?

Supplementary Question 4

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa wananchi wa Yulansori, Lelembo wanapata shida kubwa ya barabara na Halmashauri haina uwezo kama ilivyo kwa wananchi wa Mpwapwa na kwa bahati nzuri Waziri wa TAMISEMI alishatembelea maeneo hayo, je, Serikali ina kauli gani kuwasaidia wananchi hawa ambao ni wazalishaji wakubwa wa mazao ya mahindi, alizeti na vitunguu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nilifika maeneo yale mimi na Mbunge tumetembelea barabara ile yenye kilometa 25.2. Kwa sababu changamoto za barabara ile ni kubwa kwani mmomonyoko umekuwa mkubwa kwa bajeti ya kawaida imekuwa ni jambo kubwa sana. Tuliwaelekeza wataalam wafanye upembuzi yakinifu wa barabara ile na inaonekana kuna madaraja na ukibadilisha kuweka tabaka la kifusi, bahati nzuri taarifa hizo zipo katika Ofisi yetu na katika mpango wa bajeti wa mwaka 208/2019 barabara ile ni miongoni mwa barabara za kipaumbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mwaka huu unaokuja barabara ile tunaenda kuishughulikia. (Makofi)

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:- Barabara ya kutoka Mima hadi Mkanana ni mbaya sana na inapitika kwa shida sana wakati wote; na Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa haina uwezo kifedha wa kuifanyia mategenezo makubwa:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuifanyia matengenezo makubwa barabara hiyo ili iweze kupitika wakati wote?

Supplementary Question 5

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa barabara inayounganisha Mkoa wa Iringa na Morogoro ni moja tu inapitia Kitonga; na kwa kuwa hoja hii nilishawahi kuileta kwamba siku itakapotokea barabara ya Kitonga imefunga kwenda Zambia na Afrika ya Kusini itabidi watu wazunguke Dodoma. Kwa kuwa wananchi wa Kilolo wa Kata ya Muhanga, Masisiwe, Idete, Itonya, Kimala wameanza kwa makusudi kabisa kupasua barabara ambayo Serikali ilishaahidi kuunganisha Mkoa wa Morogoro na kutokea kwa Mheshimiwa Susan Kiwanga, wamefanya jitihada kubwa, je, Mheshimiwa Waziri atakubali kuitembelea na kutuunga mkono ili wananchi waweze kupata nguvu na kuimalizia barabara hiyo? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, nilivyofika katika Halmashauri na Jimbo la Kilolo, Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Kilolo walizungumzia concern ya barabara hiyo. Kwa sababu jukumu letu kama Serikali ni kubwa ni kutoa huduma kwa wananchi, nami nilieleza wazi kwamba ni jukumu la Serikali kushughulikia barabara hii. Kwa sababu barabara hii itadondokea kwa wenzetu wa TANROARD, lakini ni Serikali yetu yote kwa ujumla, tutaangalia nini cha kufanya kwa ajili ya kuipa kipaumbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli pia siku ile wananchi walisema endapo barabara ile ikijifunga watashindwa kusafiri lakini hatuwezi kutoa ahadi ya moja kwa moja hapa. Niseme Serikali tumelichukua kwa ujumla wake na kuliweka miongoni mwa mipango mikakati ili siku za usoni barabara ile ikiwezekana tuiboreshe kwa huduma pana ya wananchi wa Tanzania lakini hata nchi jirani.