Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 50 2018-04-10

Name

Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. KHATIB SAID HAJI aliuliza:-
Kuchelewesha haki ni kunyima haki.
Je, Jeshi la Polisi limejitathmini juu ya utendaji wake, hususan katika Idara ya Upelelezi wa Makosa mbalimbali kabla ya kuyafikisha mashtaka mahakamani?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Khatib Said Haji, Mbunge wa Konde, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, upelelezi wa makosa ya jinai unafanywa kwa kuzingatia sheria mbalimbali kama vile Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Sura ya 20 Marejeo ya mwaka 2002, Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 Marejeo mwaka 2002 na Sheria ya Ushahidi Sura ya 6 Marejeo ya mwaka 2002, pamoja na kuzingatia kanuni za kiutendaji za Jeshi la Polisi (Police General Orders) na sheria nyingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, moja ya lengo la upelelezi wa makosa ya jinai ni kukusanya ushahidi utakaothibitisha kosa lililotendeka na kuripotiwa kituoni. Aidha, kuna baadhi ya makosa yaliyotendeka huhitaji muda mrefu ili ushahidi wake kuweza kupatikana, mathalani makosa ya mauaji na yanayofanana na hayo. Inapodhihirika kuwa kuna ushahidi uliopatikana unaweza kuthibitisha kosa, jalada hupelekwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa hatua za kusomwa na kuandaa mashtaka pale ambapo wanaona ushahidi umejitosheleza na kupeleka mahakamani.
Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Polisi hufanya tathmini ya kutosha katika utendaji wake kupitia Kitengo cha Ndani cha Tathmini na Uangalizi (Internal Monitoring and Evaluation) na kutoka kwa Waangalizi wa Nje (External Oversight) ambao hulisaidia Jeshi la Polisi kurekebisha kasoro mbalimbali za kiutendaji.