Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 12 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 99 2018-04-18

Name

Hassanali Mohamedali Ibrahim

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiembesamaki

Primary Question

MHE. SULEIMAN A. SADDIQ (K.n.y. MHE. IBRAHIM HASSANALI RAZA) aliuliza:-
Kituo cha Polisi Mazizini kilichopo Kiembe Samaki kipo katika hali mbaya na hakina vitendea kazi, jengo ni chakavu, hakina gari na mazingira yake hayaridhishi:-
Je, ni lini Serikali itaboresha kituo hicho kwa kutatua changamoto zilizopo?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ibrahim Hassanali Raza, Mbunge wa Kiembe Samaki, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli hali na mazingira ya Kituo cha Polisi Mazizini hairidhishi kutokana na uchakavu wa jengo pamoja na uhaba wa vitendea kazi kama ilivyo kwa baadhi ya vituo katika maeneo mbalimbali. Kituo cha Polisi Mazizini kina majengo mawili. Katika mwaka 2015 Serikali ilifanya ukarabati wa jengo moja la kituo hiki ambapo ukarabati ulikamilika na tayari jengo hilo linatumika kwa kutoa huduma kwa wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mwaka wa Fedha 2018/2019, Jeshi la Polisi limependekeza kwa ajili ya maendeleo ya vituo kiasi cha shilingi bilioni 3.7 kwa ajili ya ukarabati na kuboresha miundombinu mbalimbali ya Jeshi la Polisi kote nchini ikiwemo ukarabati wa jengo la pili la Kituo cha Polisi Mazizini Jimboni Kiembe Samaki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kufanya ukarabati wa miundombinu mbalimbali ya Jeshi la Polisi na kuongeza vitendea kazi kama vile magari awamu kwa awamu ili kutatua changamoto zinazokabili Jeshi la Polisi katika maeneo mbalimbali.