Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Suleiman Ahmed Saddiq

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. SULEIMAN A. SADDIQ (K.n.y. MHE. IBRAHIM HASSANALI RAZA) aliuliza:- Kituo cha Polisi Mazizini kilichopo Kiembe Samaki kipo katika hali mbaya na hakina vitendea kazi, jengo ni chakavu, hakina gari na mazingira yake hayaridhishi:- Je, ni lini Serikali itaboresha kituo hicho kwa kutatua changamoto zilizopo?

Supplementary Question 1

MHE. SULEIMAN A. SADDIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nasafi. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Waziri na pamoja na bajeti ambayo wameipanga, lakini nina maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali ambalo limeulizwa la polisi Mazizini linafafana kabisa na suala la Mvomero katika Kituo cha Polisi Turiani. Kituo cha Polisi Turiani kipo katika jengo la mabati na jengo lile lilijengwa tokea enzi ya mkoloni na hadi leo kituo kinatumika. Hata hivyo, wananchi na wadau mbalimbali tumeamua kujenga kituo cha polisi na sasa hivi kimefikia hatua ya lenter na ujenzi huo umefanyika zaidi ya miaka kumi iliyopita. Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kutembelea Turiani na kuonesha nia yake kuweza kumalizia kituo cha polisi Turiani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mheshimiwa Waziri anafahamu kwamba Turiani ni sehemu ya Wilaya ya Mvomero migogoro ya wakulima na wafugaji ni mingi na jitihada kubwa zimefanyika. Je, yuko tayari kutusaidia gari kwa ajili ya Kituo cha Polisi Turiani?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Murad kwa jinsi ambavyo anafuatilia kwa karibu sana masuala ya wananchi wake wa Jimbo la Mvomero. Natambua Jimbo la Mvomero jiografia yake ni ya tofauti sana kwa sababu kuna baadhi ya tarafa ziko ukanda mwingine huku kama unaelekea barabara hii ya kwenda Mikumi na upande mwingine ndiko huko Turiani anakokusemea. Kwa hiyo nianze tu kwa kusema kwamba niko tayari na si mbali kutembea kituo hicho anachokisemea ili kuweza kujionea kazi nzuri ambayo wananchi wameshafanya kwa muda mrefu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, tutaweka kipaumbele kwenye upande wa kuipatia wilaya yake vitendea kazi ikiwemo gari kwa kuzingatia hali halisi ya migogoro ambayo imekuwa ikijitokeza katika Wilaya ya Mvomero pamoja na Kilosa ambayo inahitaji sana vitendea kazi kama hivyo. Kwa hiyo tunazingatia punde tutakapokuwa tumepata magari kwa ajili ya kusaidia vituo vya polisi. (Makofi)

Name

Ali Hassan Omar King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Jang'ombe

Primary Question

MHE. SULEIMAN A. SADDIQ (K.n.y. MHE. IBRAHIM HASSANALI RAZA) aliuliza:- Kituo cha Polisi Mazizini kilichopo Kiembe Samaki kipo katika hali mbaya na hakina vitendea kazi, jengo ni chakavu, hakina gari na mazingira yake hayaridhishi:- Je, ni lini Serikali itaboresha kituo hicho kwa kutatua changamoto zilizopo?

Supplementary Question 2

MHE. ALI HASSAN OMAR KING: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi. Waswahili wanasema usipoziba ufa utajenga ukuta na usipotibu utazika, swali langu dogo tu, namuuliza Mheshimiwa Waziri. Ni lini Serikali itakusanya mchango wa maafa kwa jengo bovu la Ziwani Polisi la Kilimanjaro pindi maafa hayo au jengo litakapoanguka. Ahsante.

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili limeletwa mara kadhaa. Niseme tu, kwa sababu tuna siku chache kabla hatujakwenda kwenye bajeti yetu tutapa fursa tuongee na Mheshimiwa Mbunge ili tukubaliane kuhusu ni lini kwa sababu swali lake ametaka tumtajie ni lini tutachukua hatua hiyo aliyoisema yeye.

Name

Jaku Hashim Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. SULEIMAN A. SADDIQ (K.n.y. MHE. IBRAHIM HASSANALI RAZA) aliuliza:- Kituo cha Polisi Mazizini kilichopo Kiembe Samaki kipo katika hali mbaya na hakina vitendea kazi, jengo ni chakavu, hakina gari na mazingira yake hayaridhishi:- Je, ni lini Serikali itaboresha kituo hicho kwa kutatua changamoto zilizopo?

Supplementary Question 3

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nikushukuru kwa kuniona. Nina swali dogo sana la nyongeza. Swali la msingi linahusu vituo na nilikuwa nikipigia kelele huu mwaka wa tatu au wa nne kuna mjenzi wa kampuni ya Albatina na Mheshimiwa Waziri amekuwa akiahidi sana ndani ya jengo hili muhimu kwa wananchi. Kesho kutwa tarehe mosi mwezi wa Tano Mungu akijalia tunapitisha bajeti; na nilimwambia huyu mzee mpaka leo asubuhi tumezungumza, huyu mzee bado anaumwa anadai ng’ombe kama 30; na amekiri si mara ya kwanza si mara mbili, si mara tatu, kesho kutwa sitakuja kuizuia shilingi Mungu akinijalia. Je, lini atalipwa mjenzi huyu karatasi zake na lini nimlete?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nikiri kwamba Mheshimiwa Jaku amelifuatilia sana jambo hili Ofisi na hata kwenye masuala ya anapopata fursa ya kusemea hapa kwenye bajeti. Kama nilivyosema, tutaonana naye ili tuweze kukubaliana, kwa sababu kitu ambacho kimetuchelewesha hapa katikati ilikuwa ni kwamba lazima madeni yote yafanyiwe uhakiki kabla hayajalipwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa yalikuwa yanafanyiwa uhakiki, nitaomba Mheshimiwa Jaku aridhie tuwe na kikao mimi pamoja na yeye na watendaji wangu ili tuweze kupata kwanza status ya upande wa uhakiki umefikia hatua gani. Tukishajua kwamba limeshahakikiwa liko tu kwenye hatua za kulipwa tutaweza kulifanyia uharaka kwa sababu kama anavyosema Meshimiwa Jaku mhusika anahitaji sana fedha kwa ajili ya matibabu.