Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 20 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 169 2018-05-20

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. OMARY T. MGUMBA aliuliza:-
REA I na II ilikuwa ni kupeleka miundombinu ya umeme vijijini na baadhi ya Makao Makuu ya vijiji tu na kuacha vitongoji vya vijiji husika.
Je, Serikali ina mikakati gani ya kuwapatia umeme vitongoji vyote na vijiji vilivyorukwa katika REA I na II?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Omary Tebweta Mgumba, Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa kupeleka umeme katika vijiji vyote ifikapo mwezi Juni, 2021. Katika kufikia azma hii, Serikali inatekeleza mradi wa REA awamu ya tatu kupitia maeneo yafuatayo: kwanza, grid extension unaohusu kupeleka umeme katika vijiji vyote ambavyo havikufikiwa na miundombinu ya umeme. Mradi huu wa REA III mzunguko wa kwanza umekwishaanza. Mzunguko wa kwanza unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2019 na mzunguko wa pili unatarajiwa kuanza mwezi Julai, 2019 na kukamilka mwezi Juni, 2021.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aina ya pili ya mradi wa REA ni mradi wa densification. Mradi huu umepangwa kutekelezwa katika vijiji ambavyo tayari vimefikiwa na miundombinu ya umeme lakini baadhi ya taasisi za huduma za kijamii na Vitongoji havikupata umeme wakati wa utekelezaji wa REA I na II.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aina ya tatu ni mradi wa kupeleka umeme katika vijiji nje na miundombinu ya umeme wa gridi kwa kutumia nishati jadidifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji na vitongoji vilivyorukwa wakati wa utekelezaji wa miradi ya REA I na II vitapatiwa umeme kupitia miradi ya densification na utekelezaji wa awamu ya kwanza ya miradi ya densification ulikwishaanza katika mikoa nane ya Mbeya, Songwe, Njombe, Iringa, Pwani, Tanga, Arusha na Mara. Serikali inafanya maandalizi ya densification awamu ya pili unaotarajiwa kuanza kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2018/2019.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki jumla ya vitongoji 55 vimeainishwa kwa ajili ya kupatiwa umeme kupitia densification awamu inayofuata. Mkakati wa Serikali ni kuvipatia umeme vitongoji vyote ifikapo mwezi Juni, 2021.