Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 29 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 242 2018-05-15

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO aliuliza:-
Watendaji wa Vijiji ni kada muhimu sana katika kuwahudumia wananchi walio vijijini:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia mafunzo ya mara kwa mara watumishi hawa ili kuboresha utumishi wao na utoaji huduma kwa wananchi walioko vijijini?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Edward Franz Mwalongo, Mbunge wa Njombe Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Watendaji wa Vijiji kama walivyo watumishi wengine wa umma wanapaswa kupewa mafunzo mara kwa mara ili kuboresha utendaji na kuongeza ufanisi. Mafunzo yanayotolewa kwa Watendaji wa Vijiji hujumuisha masuala ya utawala bora, mapambano dhidi ya rushwa, mapambano dhidi ya UKIMWI mahali pa kazi, maadili ya utumishi wa umma pamoja na majukumu yao katika utumishi wa umma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia ruzuku ya maendeleo kwa Serikali za Mitaa ambayo inajumuisha Mpango wa Mafunzo kwa watumishi wa kada mbalimbali, Watendaji wa Vijiji 1,840 walipewa mafunzo katika mwaka wa fedha 2016/17. Kuanzia Julai 2017 hadi Aprili 2018 kwa mwaka huu unaoendelea, Watendaji wa Vijiji 1,543 wamepewa mafunzo. Mpango huu ni endelevu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutumia fursa hii kuziagiza halmashauri zote nchini kuweka kipaumbele na kutenga bajeti ya mafunzo kwa kada hii muhimu na kuanzia mwakani tutaanza kufuatilia utekelezaji wa agizo hili ili kuhakikisha kuwa limezingatiwa na halmashauri zote wakati wa bajeti.