Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO aliuliza:- Watendaji wa Vijiji ni kada muhimu sana katika kuwahudumia wananchi walio vijijini:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia mafunzo ya mara kwa mara watumishi hawa ili kuboresha utumishi wao na utoaji huduma kwa wananchi walioko vijijini?

Supplementary Question 1

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na majibu ya Serikali ni dhahiri kwamba mafunzo haya hayafuatiliwi ndiyo maana sasa wanaagiza. Katika mafunzo yanayotolewa hayahusu mafunzo ya ukakamavu, je, Serikali iko tayari kuweka mpango wa kuwapeleka baadhi ya Watendaji wa vijiji kupata mafunzo ya JKT ili kusudi kuwaimarisha kiutumishi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, katika kutekeleza majukumu yao, Watendaji wa Vijiji wamekuwa wakipata madhara ikiwemo kudondoka na pikipiki na wengine kuumizwa na wananchi. Ni nani anayewajibika kuwalipa fidia pale wanapokuwa wamepata madhara hayo? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA):
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwalongo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la kwanza, napenda kumpongeza sana kwa sababu anahitaji sana Watendaji wetu wawe wakakamavu. Napenda kumpa taarifa na kulipa taarifa Bunge lako Tukufu kwamba wale Watendaji wote ambao walipitia JKT kwa mujibu wa sheria kabla utaratibu huo haujasimamishwa kwa muda, hao hawahitaji kupatiwa mafunzo tena kwa sababu tayari hao ni service girls and women. Kwa hiyo, wale ambao hawakupitia mafunzo hayo, tumepokea wazo lake zuri, tutaandaa utaratibu siyo lazima kuwapeleka JKT bali wanaweza wakahudhuria mafunzo ya mgambo ambayo huendeshwa na Washauri wa Mgambo katika wilaya zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali la pili kuhusu fidia, zipo Sheria za Utumishi zinazoelekeza kuhusu fidia. Kwa hiyo, suala hili kwa sababu ni la kisheria, naomba sana watumishi wote ambao wanapata ajali au kuumia kazini sheria zipo zitumike. Ahsante sana.

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO aliuliza:- Watendaji wa Vijiji ni kada muhimu sana katika kuwahudumia wananchi walio vijijini:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia mafunzo ya mara kwa mara watumishi hawa ili kuboresha utumishi wao na utoaji huduma kwa wananchi walioko vijijini?

Supplementary Question 2

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunikumbuka maana mara nyingi sikumbukwi kwenye maswali ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu liko sawasawa na la Mheshimiwa Mwalongo, ni kwamba kwenye Jimbo langu la Same Mashariki unakuta kata na vijiji hazina Watendaji, badala yake wanatumiwa Maafisa Ugani na wala wao hawana mafunzo ya kufanya kazi za utendaji. Ni lini Jimbo la Same Mashariki litasaidiwa ili tupate watendaji ambao wanakidhi hadhi ya kazi hiyo? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA):
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Naghenjwa Kaboyoka, Mbunge wa Same Mashariki, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba katika nchi tuna tatizo kubwa la Watendaji hasa ngazi ya Watendaji wa Kata na Vijiji. Maeneo/halmashauri nyingi zina upungufu mkubwa sana wa Watendaji wa Kata na Watendaji wa Vijiji. Kwa hiyo, kutokana na upungufu huo wamekuwa wakitumika maafisa, wakati mwingine Maafisa Elimu wa Kata, Maafisa Ugani, Maafisa Kilimo wanakaimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa suala hili kwa sababu tunaliweka katika utaratibu wa kuomba vibali vya utumishi, napenda kuahidi nchi nzima kwamba suala hili litakuwa limekwisha ifikapo mwaka 2020.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO aliuliza:- Watendaji wa Vijiji ni kada muhimu sana katika kuwahudumia wananchi walio vijijini:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia mafunzo ya mara kwa mara watumishi hawa ili kuboresha utumishi wao na utoaji huduma kwa wananchi walioko vijijini?

Supplementary Question 3

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kuwa pamoja na mafunzo ambayo wanapata Watendaji wa Vijiji katika utekelezaji wanakwenda kushirikiana na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, Vitongoji na Vijiji ambao wamekuwa wakilalamikia sana kuhusu maslahi yao. Napenda kujua, Serikali ina mkakati gani wa kuboresha maslahi ya Wenyeviti wa Serikali za Vijiji na Vitongoji pamoja na kupewa mafunzo kama watakayopewa Watendaji? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA):
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida Khenani, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama alivyosema kwamba tunafanya mafunzo mengi kwa ajili ya Watendaji, lakini napenda nimhakikishie kwamba mafunzo ya aina nyingi vilevile, hasa ya uongozi yamekuwa yakitolea kwa Wenyeviti wa Serikali za Vitongoji, Wenyeviti wa Serikali za Vijiji, Madiwani na viongozi wengine wa kuchaguliwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu maslahi, suala hilo kwa sababu liko katika maelekezo ya Serikali kwamba walipwe kupitia 20% zile za mapato ya ndani ya halmashauri, napenda kumuahidi kwamba mimi mwenyewe nitaanza ufuatiliaji wa karibu sana kuanzia mwaka ujao wa fedha ili kuhakikisha kwamba Wenyeviti wa Vitongoji na Vijiji wanalipwa.