Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 33 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 280 2018-05-21

Name

Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUZANA C. MGONUKULIMA aliuliza:-
Lengo la Serikali ni kuingiza fedha zote za kodi kwenye mfuko mmoja na baadaye asilimia fulani ya fedha hizo zirudishwe kwenye Halmashauri:-
Je, kwa nini isitungwe sheria ya kuibana Serikali ikiwa haitarejesha fedha hizo kwenye Miji, Halmashauri, Manispaa na Majiji?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Suzana Chogisasi Mgonukulima, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Sheria ya Bajeti ya mwaka 2015, kifungu cha 58 usimamizi wa mapato utazingatia misingi ifuatayo:-
• Mapato yote ya Serikali kuingizwa kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali;
• Yeyote aliyepewa mamlaka ya kukusanya mapato ya Serikali atawajibika ipasavyo katika ukusanyaji wenye ufanisi, utunzaji wa hesabu, utoaji wa taarifa na kuzuia ufujaji wa mapato; na
• Mapato yote kuingizwa kwenye Sheria ya Kuidhinisha Matumizi ya Fedha za Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kwa mujibu wa kifungu cha 44 cha Sheria ya Bajeti, mgawo wa fedha utazingatia bajeti iliyoidhinishwa, upatikanaji na mtitiriko wa fedha, utekelezaji wake, mpango wa manunuzi na mpango wa kuajiri. Aidha, hakuna fungu litakaloruhusiwa kufanya matumizi ya aina yoyote mpaka kuwe na fedha za kulipia matumizi husika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa vifungu vya 44 na 58 vya Sheria vya Bajeti vya Mwaka 2015, usimamizi wa mapato na matumizi ya Serikali umebainishwa vizuri na hivyo hakuna haja ya kutunga sheria nyingine ya kuibana Serikali ikiwa haitapeleka fedha kwenye Miji, Halmashauri, Manispaa na Majiji.