Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 35 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 301 2018-05-23

Name

Lameck Okambo Airo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE (K.n.y. LAMECK O. AIRO) aliuliza:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Rorya ilianzishwa mwaka 2007 na ina ukubwa wa kilometa za mraba 9,345 na idadi ya watu wapatao 400,000, lakini inakabiliwa na tatizo la uhaba wa watumishi katika Mahakama za Mwanzo za Kineri, Ryagoro, Obilinju na Shirati; hadi sasa Wilaya ya Rorya inatumia Mahakama ya Wilaya ya Tarime hali inayosababisha kesi kuchelewa kusikilizwa kwa wakati:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Mahakama ya Wilaya kwenye Jimbo la Rorya?

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Lameck Okambo Airo, Mbunge wa Rorya, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mpango wa Mahakama wa kujenga na kukarabati majengo ya Mahakama katika ngazi mbalimbali, Mahakama ya Wilaya ya Rorya imepangiwa kujengwa katika Mwaka wa Fedha 2019/2020.