Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 35 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 302 2018-05-23

Name

Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. STEPHEN H. NGONYANI aliuliza:-
Katika Kata ya Magoma, Korogwe Vijijini kumejengwa Mahakama ya Mwanzo ya Kisasa, lakini toka ijengwe imefika miaka saba sasa haijafunguliwa:-
Je, ni lini Serikali itafungua Mahakama hiyo ili wananchi waachane na usumbufu wa kufuata huduma za Mahakama Korogwe?

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stephen Hillary Ngonyani, Mbunge wa Korogwe Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Mahakama ya Mwanzo ya Magoma ilijengwa muda mrefu kama anavyosema Mheshimiwa Mbunge wa Korogwe, lakini jengo lile halikukamilika. Mahakama iliyojengwa ni ya kisasa, iliyohusisha ujenzi wa jengo la Mahakama, nyumba ya Hakimu na kantini.
Mheshimiwa Naibu Spika, majengo haya yalisimama kwa muda mrefu kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa fedha. Mradi huu sasa umefufuliwa na unatekelezwa na SUMA JKT, chini ya usimamizi wa TBA Mkoa wa Tanga na unatarajiwa kukamilika na kuanza kutumika kabla ya Julai mwaka huu 2018.