Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 12 2018-09-04

Name

Bhagwanji Maganlal Meisuria

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Primary Question

MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA aliuliza:-
Je, lini Serikali itapeleka gari, radio call pamoja na vitendea kazi vingine katika Kituo cha Polisi cha Chwaka na Jozani?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bhagwanji Maganlal Meisuria, Mbunge wa Chwaka, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uhaba wa magari pamoja na vitendea kazi katika Vituo vya Polisi nchini kikiwemo Kituo cha Polisi Chwaka na Jozani. Hata hivyo, Jeshi la Polisi linaendelea na mchakato wa upatikanaji wa magari mapya yaliyonunuliwa na Serikali. Baada ya mchakato huu kukamilika, hatua za kuyagawa zitafuata kwa kuzingatia kiwango cha uhalifu katika maeneo husika, idadi ya watu na ukubwa wa eneo la doria.
Mheshimiwa Spika, Kituo cha Polisi Chwaka kinatumia mawasiliano ya radio ya mezani kwa sababu umbali wa ilikofungwa mitambo ya mawasiliano ya radio za mkononi. Aidha, radio za mezani kwa ajili ya Kituo cha Polisi Jozani imekwishapatikana na mafundi wa Radio za Polisi wanamalizia ufungaji wake ili kurejesha mawasiliano ya uhakika katika eneo hilo.
Mheshimiwa Spika, ni azma ya Serikali kuhakikisha kuwa inaboresha mawasiliano katika vituo vyote vya Polisi nchini kwa kutafuta repeaters (mitambo wa radio za mkononi) ambazo zitafungwa katika vituo visivyokuwa na mawasiliano ya radio za mkononi ikiwemo Chwaka na Jozani.