Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 53 2018-09-10

Name

Haroon Mulla Pirmohamed

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA (K.n.y. MHE. HAROON M. PIRMOHAMED) aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itafanyia ukarabati barabara za Mahongole – Kilambo kilometa 20, Igurusi – Utengule kilometa 22, Chimala – Kapunga kilometa 25 na Mlangali – Ukwavila kilometa 23?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Haroon Mulla Pirmohamed, Mbunge wa Mbarali, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali ina mtandao wa barabara wenye urefu wa kilometa 685 zinazohudumiwa na Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA), kilometa 341 ni za kiwango cha changarawe na kilometa 344.5 ni za udongo.
Katika mwaka wa fedha 2017/2018 Serikali ilipeleka jumla ya shilingi bilioni 1.065 sawa na asilimia 91 ya bajeti iliyopangwa kwa ajili ya matengenezo ya barabara na madaraja katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali. Kazi zilizofanyika ni pamoja na ukarabati wa Madaraja ya Mporo III, Mporo IV na Manienga. Matengenezo ya barabara zenye urefu wa kilometa 50 kwa kiwango cha changarawe, ukarabati wa sehemu korofi zenye jumla ya kilometa 30 na matengenezo ya kawaida kwenye barabara zenye urefu wa kilometa 67.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2018/2019 Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali imetengewa kiasi cha shilingi milioni 220 kwa ajili ya matengenezo maalum katika barabara ya Mlangali – Uturo- Ukwavila na Chimala-Kapunga kwa eneo korofi lenye jumla ya kilometa 11. Vilevile Halmashauri imetengewa shilingi milioni 12.18 kwa ajili ya matengenezo ya makalavati 21 katika barabara ya Igalako- Mwatenga - Kilambo.