Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 54 2018-09-10

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:-
Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ina jumla ya kata 39 na vijiji 157. Halmashauri iliomba kuigawa Wilaya hiyo ambayo ina ukubwa zaidi ya Mkoa wa Mtwara wenye Wilaya sita:-
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuigawa Wilaya ya Tunduru ili iwe rahisi kutoa huduma karibu zaidi na wananchi?
(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuzigawa Kata za Mchoteka, Mtina, Namasakala, Lukumbule, Mchasi, Tuwemacho na Misechela ambazo zina wakazi zaidi ya 30,000 kila Kata?
(c) Je, Serikali itaidhinisha lini mgao wa vijiji uliopendekezwa na Halmashauri mwaka 2015 ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ofisi ya Rais, TAMISEMI napenda kujibu swali la Mheshimiwa Daimu Iddi Mpakate, Mbunge wa Tunduru Kusini, lenye sehemu (a), (b) na (c) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, taratibu za kuanzisha au kugawanya maeneo ya kiutawala zimeainishwa kwenye Sheria ya Serikali za Mitaa Sura ya 287, pamoja na Mwongozo wa Serikali wa mwaka 2014.
Mheshimiwa Spika, maombi ya kugawa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru na kuanzisha Halmashauri ya Wilaya ya Nalasi na kuzigawa Kata za Mchoteka, Mtina, Namasakala, Lukumbule, Mchasi, Tuwemacho na Msecheke yaliwasilishwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI yakiwa pamoja na ombi la kuanzisha mkoa mpya wa Selous. Serikali imetafakari maombi haya na kuyaona kuwa ni ya msingi, hata hivyo, kutokana na changamoto ya kuimarisha kwanza miundombinu kama majengo ya ofisi na nyumba za watumishi na mahitaji mengine kama vifaa vya ofisi, watumishi wa kutosha na vyombo vya usafiri kwenye maeneo mapya ya utawala yaliyoanzishwa tangu mwaka 2010 na 2012, Serikali imesitisha uanzishwaji ya maeneo mapya ya utawala hadi yaliyopo yaimarishwe kikamilifu.