Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 5 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 58 2018-09-10

Name

Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO (K.n.y MHE. DEVOTHA M.
MINJA) aliuliza:-
Viwanja vingi vya michezo vinavyomilikiwa na Chama cha Mapinduzi vimechakaa kutokana na kutoendelezwa kwa muda mrefu. Mfano, Kiwanja cha SabaSaba Mkoani Morogoro.
Je, Serikali haioni kuna haja ya kubinafsisha viwanja hivyo ili viendelee kutumika katika michezo?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Devotha Mathew Minja, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Sera ya Maendeleo ya Michezo ya mwaka 1995 inaelekeza kuwa utunzaji wa viwanja utafanywa na taasisi zinazomiki viwanja hivyo. Kwa hiyo, viwanja vinavyomilikiwa na Chama cha Mapinduzi mfano kiwanja cha SabaSaba katika Manispaa ya Morogoro ni sawa na viwanja vingine vya michezo vya taasisi binafsi, mashirika ya umma, vilabu na vyama vya michezo. Hivyo, suala la utunzaji na ukarabati vinabakia kuwa jukumu la mmiliki.
Mheshimiwa Spika, viwanja vyote bila kujali mmiliki wake vinatakiwa kutunzwa vizuri ili vitumike kulingana na makusudio yake. Pale ambapo uwezo haupo inashauriwa kutafuta wabia na wafadhili ili wananchi waendelee kunufaika na rasilimali hiyo.