Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO (K.n.y MHE. DEVOTHA M. MINJA) aliuliza:- Viwanja vingi vya michezo vinavyomilikiwa na Chama cha Mapinduzi vimechakaa kutokana na kutoendelezwa kwa muda mrefu. Mfano, Kiwanja cha SabaSaba Mkoani Morogoro. Je, Serikali haioni kuna haja ya kubinafsisha viwanja hivyo ili viendelee kutumika katika michezo?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Chama cha Mapinduzi kimeshindwa kuendeleza viwanja vingi vya michezo, ikiwemo kiwanja cha Nangwanda Sijaona katika Manispaaa ya Mtwara Mikindani.
Je, Serikali haioni sasa ni wakati mwafaka wa kurudisha viwanja hivyo Halmashauri kama ilivyofanya kwenye mashamba yasiyoendelezwa ya watu binafsi? (Makofi)
Swali langu la pili, kwa kuwa michezo ni afya, michezo ni ajira, na michezo ni furaha. Kwa kuwa chama cha Mapinduzi kimeshindwa kuviendeleza viwanja hivi na kuwafanya wanamichezo wetu wacheze katika mazingira duni...
Mheshimiwa Spika, naomba unisikilize. Michezo ni afya, ni furaha na ni ajira. Kwa kuwa, Chama cha Mapinduzi kimeshindwa kuviendeleza viwanja hivi hatuoni kwamba Chama cha Mapinduzi kina nia ya kudunisha wanamichezo wetu kwa sababu wanapata ajali mbalimbali wanapokuwa wanachezea katika viwanja hivyo? Nakushukuru. (Makofi)

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nikuhakikishie kupitia Bunge lako tukufu kwamba, siyo kweli kwamba CCM imeshindwa kwa sababu asilimia 99 ya michezo yote nchini inaendeshwa kwenye viwanja hivyo, sasa kushindwa huko kukoje? Sasa hivi tunaanza Ligi Kuu ya Tanzania na sehemu kubwa ya michezo hiyo itachezwa kwenye viwanja hivyo hivyo.
Mheshimiwa Spika, nakubaliana na wewe kwamba vingi haviko kwenye hali nzuri sana na Wizara ilikuwa imeiachia Shirikisho la Soka nchini kufanya majadiliano na wenye viwanja, sasa tumeona maendeleo siyo ya kasi ya kutosha, Wizara imeamua yenyewe sasa siyo tu kwa kushirikisha Shirikisho la Soka nchini, mashirikisho yote ya michezo nchini, kukaa pamoja na wamiliki tuweze kukubaliana namna ya kuboresha hivi viwanja na kuweza kupata misaada ambayo kwa kawaida itakwenda kwa urahisi zaidi kwa taasisi ambazo zina ubia na Serikali. Tunataka watuachie ubia wawe na ubia na Serikali ili tuweze kurabati viwanja, kama ambavo FIFA ilivyoweza kukarabati Kiwanja cha Kaitaba na Kiwanja cha Nyamagana.

Name

Rev. Peter Simon Msigwa

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO (K.n.y MHE. DEVOTHA M. MINJA) aliuliza:- Viwanja vingi vya michezo vinavyomilikiwa na Chama cha Mapinduzi vimechakaa kutokana na kutoendelezwa kwa muda mrefu. Mfano, Kiwanja cha SabaSaba Mkoani Morogoro. Je, Serikali haioni kuna haja ya kubinafsisha viwanja hivyo ili viendelee kutumika katika michezo?

Supplementary Question 2

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Swali langu kwa Mheshimiwa Waziri pamoja na majibu yake ya swali la msingi, tukumbuke kwamba viwanja hivi vilitengwa wakati mfumo wa chama kimoja na maeneo mengi yalitengwa na wakoloni, kwa maana ya kwamba wananchi wote wafaidike na maeneo hayo. Chama cha Mapinduzi kime-take advantage na kwa kweli kimekuwa hakiendelezi hivyo viwanja.
Mheshimiwa Spika, hamuoni kwamba mnapingana na sera yenu ya kutenda haki na usawa katika nchi kwa kuendelea kupora na kunyang’anya hivo viwanja, kuwadhulumu Watanzania wote ambao walishiriki kutengeneza na kuviandaa viwanja hivyo?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, viwanja hivi havikuporwa kwa mtu yeyote, hii dhana ya kuporwa inaondoka kabisa kwenye swali la msingi alilouliza Mheshimiwa Devotha Minja.
Mheshimiwa Spika, naomba tu kukuhakikishia tu kwamba kama kuna hoja ya msingi kwamba kuna kuporwa, maana kuporwa is a criminal act, basi naomba hili suala lifikishwe Mahakamani ili liweze kuamuliwa inavyostahili. (Makofi)