Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 5 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 60 2018-09-10

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itafungua Ofisi za TANESCO Wilayani Kyerwa ili kuwafikishia karibu wananchi huduma zitolewazo na TANESCO, kama vile kununua umeme, kubadilisha mita na huduma nyingine?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Sebba Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, katika hatua ya kuboresha huduma kwa wateja Shirika la Umeme nchini (TANESCO) kupitia bajeti ya mwaka 2018/2019 inajenga Ofisi ya TANESCO Wilaya ya Kyerwa katika Kiwanja Na. 210 C, kilichopo eneo la Rwenkorongo. Kazi ya ujenzi wa ofisi hiyo inaendelea vizuri na inatarajia kukamika mwezi Januari, 2019.
Mheshimiwa Spika, katika hatua za muda mfupi TANESCO imefungua ofisi katika Mji wa Nkwenda, kwa ajili ya kuwahudumia wateja wakati kazi ya ujenzi wa ofisi mpya inaendelea. Kwa sasa Meneja wa TANESCO Wilaya ya Misenyi pamoja watumishi wengine watatu, wanaendelea kutoa huduma kwa wateja wa maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Kyerwa kupitia ofisi hiyo. Ahsante.