Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 99 2018-09-13

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza:-
Je, Serikali itapeleka lini gari la wagonjwa kwenye Kituo cha Afya Chiwale kwani ni zaidi ya miaka miwili sasa baada ya gari lililokuwepo kuungua moto?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecil David Mwambe, Mbunge wa Ndanda kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya Chiwale ni moja kati ya vituo vya kutolea huduma za afya 33 vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Ni kweli gari la wagonjwa la Kituo cha Afya Chiwale lilichomwa moto na wananchi mwaka 2013, suala hili lilisababisha kituo hicho kukosa gari la wagonjwa kwa muda mrefu na hivyo kusababisha usumbufu mkubwa kwa wagonjwa wanaohitaji huduma za rufaa.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, Halmashauri ya Wilaya ya Masasi imefanya jitihada za kuhakikisha huduma za dharura kwa wagonjwa wanaohitaji rufaa hazikwami kwa kutoa gari lililokuwa linatumiwa na timu ya Menejimenti ya Afya ya Halmashauri ya Wilaya ya Masasi (CHMT). Aidha, Halmashauri ya Wilaya ya Masasi imepewa maelekezo na Ofisi ya Rais, TAMISEMI kutenga fedha kwenye bajeti kwa ajili ya kununua gari la wagonjwa ili kuwaondolea wananchi usumbufu.