Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 8 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 102 2018-09-13

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA (K.n.y. MHE. MHE.ANNA R. LUPEMBE) aliuliza:-
Je, ni lini Redio Tanzania (TBC) itasikika katika Kata za Ilela na Ilunde Wilayani Mlele?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (MHE. ANTHONY P. MAVUNDE K.n.y. WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Anna Richard Lupembe, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TBC imeendelea na jitihada za kupanua usikivu katika Mikoa na Wilaya ambazo bado hazina usikivu au kuwa na usikivu hafifu wa redio. Katiba bajeti ya mwaka 2016/2017 TBC ilitengewa kiasi cha shilingi bilioni moja kwa ajili ya upanuzi wa usikivu katika Wilaya tano za mpakani mwa nchi. Maeneo ambayo mitambo imefungwa na matangazo ya redio kuwashwa ni Rombo, Nyasa, Tarime, Kibondo na Namanga. Serikali inaendelea na utaratibu huo wa kuongeza usikivu kwenye maeneo yasiyo na usikivu mzuri katika Mikoa ya Katavi, Njombe, Simiyu na Songwe.
Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali ni kujenga mitambo ya redio katika Mikoa hii katika bajeti ya mwaka 2019/2020 na katika bajeti ya mwaka 2018/2019 TBC imetengewa kiasi cha shilingi bilioni tano kwa ajili ya ujenzi wa studio za redio na television Makao Makuu ya nchi Jijini Dodoma.