Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA (K.n.y. MHE. MHE.ANNA R. LUPEMBE) aliuliza:- Je, ni lini Redio Tanzania (TBC) itasikika katika Kata za Ilela na Ilunde Wilayani Mlele?

Supplementary Question 1

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Spika, ahsante.
Mheshimiwa Spika, haisikiki. Nashukuru sana. Ninayo maswali mawili ya nyongeza. Ukiangalia swali la Mheshimiwa Anna Richard Lupembe angependa kujua hasa kwa Kata za Ilela na Ilunde nini kinafanyika? Sasa pamoja na kwamba Katavi imetajwa na mipango ipi, ni nini hasa kinaandaliwa kufanywa katika maeneo hayo na ni shilingi ngapi zimetengwa?
Swali la pili; kwa kuwa katika Wilaya ya Karagwe, Biharamulo, Ngara pamoja na Misenyi, TBC haisikiki na wananchi wangependa kuisikia, ni nini kinafanyika kuwezesha TBC kusikika katika maeneo hayo? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (MHE. ANTHONY P. MAVUNDE K.n.y. WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO): Mheshimiwa Spika, nikianza na swali la kwanza; katika majibu yangu ya msingi, nimeuzungumzia Mkoa wa Katavi kwa ujumla ambao tafsiri yake ni kwamba itajumuisha pia Kata za Ilunde na Ilele ambazo ziko ndani ya Mkoa wa Katavi.
Mheshimiwa Spika, kwa kipindi cha bajeti ya mwaka 2017/2018 Wizara ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo tumetengewa kiasi cha shilingi bilioni 33.2 ambapo mpango mkakati tulionao hivi sasa ni kuhakikisha kwamba tunaongeza zaidi usikivu kwa sababu ukiangalia katika mwaka 2016 TBC ilikuwa ina usikivu wa asilimia 54 tu nchi nzima.
Mheshimiwa Spika, ndani ya miaka miwili baada ya bajeti hii kuongezeka, tumefikia usikivu wa asilimia 64. Mkakati uliopo ni kuyafikia maeneo mengi zaidi ili wananchi wapate fursa ya kupata habari kupitia TBC.
Mheshimiwa Spika, nikienda katika swali la pili la katika maeneo ya Misenyi, jibu langu ni hili hili la kwamba kwa mwaka huu wa fedha ambapo tuna kiasi cha fedha nilichokisema hapo tulichotengewa, kazi yetu kubwa ni kuhakikisha kwamba tunaendelea kufunga mitambo mingi zaidi ili wananchi wapate fursa ya kuweza kusikia TBC.
Mheshimiwa Spika, katika maeneo yale ya pembezoni tumeongeza usikivu kutoka kilowati 200 mpaka kilowati 1000 na ninaamini kabisa kwamba kwa mwaka huu wa fedha tutajipanga vizuri zaidi kuhakikisha kwamba wananchi wengi wanaisikia TBC.