Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 106 2018-09-13

Name

Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:-
Polisi wanapowakamata watuhumiwa baadhi wanawaweka ndani kwa saa 24 na wengine zaidi ya saa 24.
• Je, ni makosa yapi mtuhumiwa anaweza kuwekwa ndani zaidi ya masaa 24?
• Je, ni makosa yapi ambayo mtuhumiwa anaweza kuwekwa ndani chini ya saa 24?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mattar Ali Salum, Mbunge wa Shaurimoyo lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, Sura ya 20, kifungu cha 148(5)(a) mpaka (e) kinaeleza makosa mabayo mtuhimiwa anaweza kuwekwa kizuizini zaidi ya saa 24. Makosa hayo ni kama vile uhaini, mauaji, ujambazi wa kutumia silaha, kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya, ugaidi, usafirishaji wa fedha haramu, mtuhumiwa aliyewahi kuhukumiwa kifungo kinachozidi miaka mitatu ama aliwahi kuruka dhamana na mengineyo.
Mheshimiwa Spika, makosa ambayo mtuhumiwa anaweza kuwekwa ndani chini ya saa 24 ni makosa yote isipokuwa yaliyoainishwa katika kifungu cha 148(5)(a) mpaka (f).