Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:- Polisi wanapowakamata watuhumiwa baadhi wanawaweka ndani kwa saa 24 na wengine zaidi ya saa 24. • Je, ni makosa yapi mtuhumiwa anaweza kuwekwa ndani zaidi ya masaa 24? • Je, ni makosa yapi ambayo mtuhumiwa anaweza kuwekwa ndani chini ya saa 24?

Supplementary Question 1

MHE. MATTAR ALI SALUM: Mheshimiwa Spika, ahsante. Namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Alhaji Masauni.
Mheshimiwa Spika, wapo askari wanaowaweka ndani watuhumiwa zaidi ya saa 24 wakati hawana makosa ya kuwekwa ndani zaidi ya saa 24. Serikali inawachukulia hatua gani askari hawa wakibainika wanakiuka Sheria za Jeshi la Polisi?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, Watanzania wengi hawana elimu ya Sheria ya Jeshi la Polisi. Serikali ina mkakati gani wa kutoa elimu ili Watanzania wakafahamu haki yao ya kimsingi ili waweze kujua taratibu za kuwekwa ndani zaidi ya saa 24 na sheria ambazo haziwahusu kuwekwa ndani zaidi ya saa 24? Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Spika, nataka nimjibu Mheshimiwa Mattar kwamba sheria niliyoizungumza inahusisha watu wenye makosa ya aina ambayo nimeyataja.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kama kutakuwa kuna Askari Polisi ambaye amemweka mtu ndani na hakufanya makosa ambayo nimeyataja, naye Mheshimiwa Mattar anamfahamu, basi ni wajibu wake kuweza kuwasilisha taarifa hiyo ili tuweze kuchukua hatua kama ambavyo tumefanya kwa askari wengine wenye makosa mbalimbali.
Mheshimiwa Spika, kwa mfano, katika kipindi cha miezi sita ya mwaka huu, takriban askari 15 ambao walifanya makosa ya kukiuka maadili ya utendaji wao wa kazi ambao tumeweza kupokea taarifa zao na kati ya hao mpaka sasa hivi tayari askari wawili wameshachukuliwa hatua. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mattar kama ana taarifa hizo aziwasilishe katika mamlaka husika ili hatua ziweze kuchukuliwa.
Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, suala la elimu linaendelea kutolewa na ni wajibu wa kila mtu akiwemo yeye Mheshimiwa Mbunge kuweza kutusaidia kutoa elimu kwa wananchi wake, ingawa kutokufahamu sheria hakuhalalishi juu ya uvunjifu wa sheria.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi kwamba tutaendelea kujitahidi kadri itakavyowezekana watusaidie Waheshimiwa Wabunge akiwemo Mheshimiwa Mattar kutoa elimu kwa jamii kuhusiana na ufahamu wa sheria mbalimbali katika nchi yetu. (Makofi)

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba niongezee majibu ya nyongeza kwenye majibu mazuri ambayo Mheshimiwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ameyasema.
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kulikuwa na malalamiko kwa wananchi kwa kuwekwa ndani na baadhi ya askari ambao sio waaminifu, siyo waadilifu kwenye makosa ambayo hayastahili, lakini pia wamekuwa wakiwaweka ndani baadhi ya wananchi kwenye makosa ambayo pia hayahitajiki hata kuwekwa ndani, hata nusu dakika au sekunde.
Mheshimiwa Spika, tayari nimeshatoa maelekezo kwamba Makamanda wote wa Polisi wa Mikoa na Wakuu wa Polisi wa Wilaya, kituo chochote ambacho kitaonekana na malalamiko ya kukiuka utaratibu huu wa kuweka wananchi ndani, viongozi hao watawajibika. Hivi karibuni nitaanza ziara kwenye mikoa yote ya Tanzania pale ambapo nitakuta vituo, askari bado wanalalamikiwa, askari hao hawatakuwa na nafasi ya kuendelea kulichafua Jeshi zuri la Polisi ya nchi yetu.(Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:- Polisi wanapowakamata watuhumiwa baadhi wanawaweka ndani kwa saa 24 na wengine zaidi ya saa 24. • Je, ni makosa yapi mtuhumiwa anaweza kuwekwa ndani zaidi ya masaa 24? • Je, ni makosa yapi ambayo mtuhumiwa anaweza kuwekwa ndani chini ya saa 24?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri amejibu kwamba ikigundulika askari wanaowaweka kituoni wananchi kwa muda watachukuliwa hatua. Wakati nachangia bajeti iliyopita ya Wizara ya Mambo ya Ndani nilieleza bayana kabisa kwamba kuna baadhi ya mahabusu kituo cha Kawe waliwekwa ndani kwa zaidi ya miezi mitatu na nikasema kabisa na nikamtaja na askari aliyehusika mpaka leo hajachukuliwa hatua.
Je, ni kwa nini Mawaziri wanatumika kwenye Bunge Tukufu kuwadanganya watanzania bila kuchukua hatua?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na hii hoja ya mahabusu Kituo cha Kawe, tulishawahi kutoa maelekezo, uchunguzi ufanyike ili hatua ziweze kuchukuliwa, lakini kama Mheshimiwa Mbunge atataka kulithibitishia Bunge hili tukufu mpaka kama hatua hazijachukuliwa, basi nimuahidi kwamba nitakapotoka hapa nitafuatilia nijue ni kwa nini hatua kama hazijachukuliwa ama pengine wanastahili kuendelea kukaa ndani kwa mujibu wa sheria.

Name

John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:- Polisi wanapowakamata watuhumiwa baadhi wanawaweka ndani kwa saa 24 na wengine zaidi ya saa 24. • Je, ni makosa yapi mtuhumiwa anaweza kuwekwa ndani zaidi ya masaa 24? • Je, ni makosa yapi ambayo mtuhumiwa anaweza kuwekwa ndani chini ya saa 24?

Supplementary Question 3

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Spika, ninafikiri kwamba ni vema Mawaziri wetu wanapokuja kutoa majibu hapa wajue Watanzania wanawaangalia na Watanzania wanasikitika sana pale wanapokuwa wanatoa taarifa ambazo siyo za kweli. Kwa mfano, juzi amekamatwa Mwenyekiti wa Kijiji anaitwa Tanzania Omutima, Kijiji cha Kewanja kwa tuhuma tu, amekaa siku nne hajafikishwa Mahakamani na wala hajapelekwa polisi. Pia amekamatwa kijana anaitwa Mudude Nyagali, amewekwa ndani zaidi ya siku 30.
Mheshimiwa Spika, ninachoomba Waziri atoe tamko kwamba ni marufuku kuanzia sasa watu wa abide na sheria, kukamata mtu na kukaa naye zaidi ya yale masaa ambayo sheria inaruhusu kama mtu amefanya hivyo afikishwe kwenye utaratibu, ashitakiwe kwa kukiuka sheria ambayo tunayo mpaka sasa.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Spika, kwanza napingana kabisa na kauli yake kwamba Mawaziri hapa tunatoa majibu ambayo siyo sahihi. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, majibu ambayo tunayotoa hapa ni majibu ambayo tumeyafanyia utafiti wa kina na tunajiamini kwamba tunachokizungumza hapa ni kitu ambacho ni sahihi kwa kiwango kikubwa sana.
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge anataka tutoe tamko, matamko tumekuwa tukitoa kila siku na siyo lazima atoe matamko kwa sababu sheria zinajulikana, tunachokifanya ni kusimamia sheria ambazo tumezitunga humu Bungeni na Mheshimiwa Heche anazifahamu. Kwa hiyo, iko wazi kwamba yeyote ambaye hafuati sheria na hakuna ambaye yuko juu ya sheria, ikiwemo Wasimamizi wa Sheria ambao ni Vyombo ya dola.
Mheshimiwa Spika, tunasema kila siku kwamba kama kuna Askari yeyote ambaye anatumia nafasi yake vibaya kinyume na maadili yake ya kazi, tutamchukulia hatua na tumekuwa tukifanya hivyo, tukiwachukulia na tutaendelea kufanya hivyo. (Makofi)

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri juu ya swali ambalo limeulizwa na Mheshimiwa Heche.
Mheshimiwa Spika, pengine nitoe fursa ya kuelimisha kidogo hii dhana ya saa 24 kukaa mahabusu. Kwenye Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, unapomkamata kwa mara ya kwanza mtuhumiwa na kumuweka mahabusu, kwa maana ya matakwa ya saa 24. Saa 24 yale yanaendana na upelelezi wa awali. Kuna mazingira ambapo uliyemweka ndani hata kabla ya saa 24 hayajafika mtamtoa ndani katika upelelezi ama kuna mahala anaenda kuonesha silaha, ama kuna mahala anaenda kuonesha ushahidi fulani kutokana na maelezo yake. Mnapotoa atakaporudi mahabusu huyo mtuhumiwa anaanza kuhesabiwa masaa yake upya. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa bahati mbaya wananchi wanahesabu tangu alipokamatwa, lakini kisheria tunahesabu tofauti. Kwa hiyo, nimuelimishe Mheshimiwa Heche, huyo anayemsema Mwenyekiti wa Kijiji ambaye aliyekamatwa pale Nata, kulikuwa na masuala ya vielelezo vya documents kwa sababu fedha za kijiji zaidi ya shilingi milioni 300, vilevile ilikuwa inahusisha na Kampuni ya Uwekezaji wa Grument. Kwa hiyo, aliyekuwa amekamatwa tulitoa maelekezo. Mheshimiwa Heche dhana hii muifahamu vizuri ya masaa 24.
Mheshimiwa Spika, nilikuwa naona wananchi waelewe dhana ya saa 24 inaanza wakati gani na inaisha wakati gani. Siyo nia ya Serikali kuwatesa wananchi wake, na ndiyo maana majibu niliyoyatoa mwanzo nilisema wale askari ambao watakiuka sheria hiyo ya kuwaweka ndani tunachukua hatua, hakuna yeyote ambaye tunamfumbia macho. Kwa hiyo, Mheshimiwa Heche uwe na amani huyo mtu unayemsema tumeshatoa maelekezo na tunajua concern yako. Ahsante sana.(Makofi)

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:- Polisi wanapowakamata watuhumiwa baadhi wanawaweka ndani kwa saa 24 na wengine zaidi ya saa 24. • Je, ni makosa yapi mtuhumiwa anaweza kuwekwa ndani zaidi ya masaa 24? • Je, ni makosa yapi ambayo mtuhumiwa anaweza kuwekwa ndani chini ya saa 24?

Supplementary Question 4

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante mimi siko mbaliā€¦
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Waziri Kangi Lugola ni awamu yake ya kwanza ya kuwa katika nafasi hii, na kwa kuwa mara nyingi nikimsikia na hata ndani ya Bunge amethibitisha ya kwamba atakomesha hiyo hali ya wananchi kuonewa, kuwekwa mahabusu muda mrefu bila utaratibu wowote.
Mheshimiwa Spika, je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari sasa kwenda kwenye mahabusu ya Wilaya ya Ifakara na Mlimba kwenda kuangalia hali halisi, mahabusu wanavyowekwa ndani muda mrefu lakini hata chakula hawapewi, mara nyingi nimeenda kuwanunulia chakula na kuwapa mahabusu haki zao zinavunjwa kabisa za kibinadamu, hilo wa kutowapa mahabusu chakula unalizungumziaje?

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwanza wananchi wa Tanzania nataka niwahakikishie kwamba siyo nia wala lengo la Jeshi la Polisi kuwatesa mahabusu wanapokuwa wamekamatwa na wako ndani. Mahabusu wote wanapata chakula na wapo watu ambao wanapewa tender hizi za kuleta vyakula kwa mahabusu, hilo la kwanza.
Mheshimiwa Spika, pili kumekuwa na wananchi pia ambao wana vyakula wanavyohitaji kuwaletea wananchi mahabusu wao. Vyakula hivyo pia tumekuwa tukiwaruhusu kuwapatia mahabusu na kwa kuwa amelenga Mlimba, kwamba kuna matatizo nimeishasema kwamba kutokana na tatizo la baadhi ya askari wachache ama kuwabambikiza kesi wananchi ama kuwatesa nimesema jambo hilo halitakuwa na nafasi na litakomeshwa. Nimesema nitaanza ziara mikoa yote hivi karibuni na hizo kero nitazishughulikia. (Makofi)

Name

Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:- Polisi wanapowakamata watuhumiwa baadhi wanawaweka ndani kwa saa 24 na wengine zaidi ya saa 24. • Je, ni makosa yapi mtuhumiwa anaweza kuwekwa ndani zaidi ya masaa 24? • Je, ni makosa yapi ambayo mtuhumiwa anaweza kuwekwa ndani chini ya saa 24?

Supplementary Question 5

MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante.
Mheshimiwa Spika, katika siku za karibuni kumejitokeza tabia chafu, mbaya na ovu kabisa ya mahabusu kufia kwenye Vituo vya Polisi. Mahabusu anapelekwa, wanashikiliwa, wanapata mateso ambayo yanapelekea vifo vyao. Hivi karibuni tu kuna baadhi ya jamii zimekataa kupokea maiti kwenda kuzika kutokana na kufia ndani ya Vituo vya Polisi.
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri anatoa kauli gani kali ya kukemea tabia hii ambayo inatia aibu nchi yetu ambayo ni ya haki na demokrasia?

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa mwananchi kufa, anakufa wakati wowote, mahali popote na ndiyo maana sijui kwenye Qurani, ila kwenye Biblia ukisoma Muhubiri 9:12 ni kwamba kifo ni mtego, kifo humnasa mtu wakati wowote, mahali popote. Kwa hiyo, mwananchi anaweza akafa akiwa polisi, anaweza akafa akiwa anafanya mapenzi, anaweza akafa akiwa kwenye gari anasafiri, anaweza akafia hata humu ndani ya Bunge. Kwa hiyo, isije ikachukuliwa kwamba anayefia kwenye Kituo cha Polisi ni kwamba ameteswa. (Kicheko)
Mheshimiwa Spika, ninakiri kwamba kumekuwa na matukio ambapo wananchi wanafia mikononi mwa polisi na pale ambapo matukio hayo yanajitokeza tumekuwa tukifanya uchunguzi na pale inapobainika kwamba polisi wamehusika tumekuwa tukichukua hatua, ndiyo maana tunazuia wananchi wasichukue sheria mikononi za kuanza kuvamia vituo kwa sababu mtu amefia mikononi mwa polisi. Nimekuwa nikihoji huyu anayekufa akifanya mapenzi mbona hawaendi kuchoma kitanda na nyumba kwamba amefia mikononi mwa kitanda? Ahsante sana. (Makofi/Kicheko)