Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 9 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 123 2018-09-14

Name

Saed Ahmed Kubenea

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Ubungo

Primary Question

MHE. SAED A. KUBENEA aliuliza:-
Kumekuwepo na vitendo vingi vya uhalifu hapa nchini kwa watu kuvamiwa, kupigwa, kujeruhiwa na kuporwa mali zao na hata kuuawa:-
• Je, Serikali ina mpango gani wa kukomesha vitendo hivyo vya uhalifu ambavyo vinatishia usalama wa raia na mali zao?
• Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza juhudi za ulinzi wa raia na mali zao ili kudumisha amani na utulivu nchini?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Saed Ahmed Kubenea, Mbunge wa Ubungo, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
i. Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Jeshi la Polisi ina mipango mbalimbali ya kukomesha vitendo vya uhalifu kwa kuimarisha doria za miguu, pikipiki na magari, pia kufanya misako dhidi ya uhalifu na wahalifu. kutoa elimu kwa jamii kuhusu mbinu za kukabiliana na uhalifu, kufanya operation za mara kwa mara na kushirikisha jamii kwenye ulinzi wa maeneo yao kupitia dhana ya Polisi Jamii.
ii. Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kufanya juhudi za kuimarisha ulinzi wa raia na mali zao kwa kuendelea kuajiri askari na kuongeza vitendea kazi pia, kwa kutumia falsafa ya kugatua madaraka. Serikali imeshapeleka wakaguzi katika tarafa, jimbo, kata, shehiya ili kushiriki kikamilifu kwa kuyabaini maeneo tete ambayo huwa ni vyanzo vya uhalifu.