Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 45 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 387 2018-06-06

Name

Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:-
Wananchi wa Kijiji cha Luganzu na majirani zao wa Ntumagu wanakabiliwa na adha kubwa ya matukio ya ujambazi pamoja na ukosefu wa Kituo cha Polisi kijijini hapo kwa ajili ya kuimarisha ulinzi. Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu hali hiyo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Oscar Rwegasira Mukasa, Mbunge wa Biharamulo kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Vijiji vya Luganzu na Ntumagu kama yalivyo maeneo mengine ya nchi kumekuwa na uhalifu mdogo na wa kawaida katika siku za hivi karibuni na hakuna tukio lolote kubwa la ujambazi ambalo limeripotiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kijiografia Vijiji vya Luganzu na Ntumagu vipo katika vituo vikubwa vya polisi vya operation vya Nyakanazi, Kalenge na Kakongo ambavyo hufanya doria za magari ya mara kwa mara katika kudhibiti uhalifu. Hali hii imepelekea wahalifu kukimbilia katika vijiji tajwa hivyo kuleta hofu na wasiwasi kwa wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kudhibiti Jeshi la Polisi limefungua kituo kidogo cha polisi katika kijiji cha Ntumagu ili kudhibiti njia ya wahalifu waliokuwa wakiingia vijijini kutokea maeneo ya Nyakanazi, Kalenge na Kakongo walikodhibitiwa.