Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 48 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 414 2018-06-11

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza:-
Tanzania inayo makabila yapatayo 124 yanaongea lugha tofauti na yanazo mila tofauti ambazo wamekuwa wakiziheshimu tangu enzi za mababu:-
(a) Je, ni lini Serikali itaandika lugha za makabila hayo ili yasiweze kupotea kwenye uso wa dunia?
(b) Je, ni lini Serikali itaandika historia kwa kila kabila nchini ili vijana wanaokua waweze kujua tamaduni za makabila yao?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Taska Restituta Mbogo, Mbunge wa Viti Maalum, lenye vipengele (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali ni msimamizi na mratibu wa shughuli mbalimbali za utamaduni nchini. Aidha, kwa mujibu wa Sera ya Utamaduni ya mwaka 1997, jamii ndiyo mmiliki wa utamaduni, hivyo wajibu wa kufanya tafiti, kuorodhesha na kuandika historia za kila jamii ni wetu sote.
Mheshimiwa Spika, Serikali kwa upande wake inaendelea na utaratibu wa kukusanya tafiti za lugha za jamii mbalimbali zinazofanywa na wadau wanaojishughulisha na ustawi wa lugha nchini na inaandaa kanzidata ili lugha hizo zisipotee kwenye uso wa dunia. Hadi sasa lugha za jamii 38 zimeshakusanywa na kufanyiwa tafiti na zimehifadhiwa kwa njia ya kamusi. Ikumbukwe kuwa lugha ni sehemu ya utamaduni wa Taifa lolote lile.
Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali na wadau mbalimbali wameandika na wataendelea kuandika historia za jamii, mila na desturi zake. Kwa sasa, karibu kila jamii imekwishaandika historia ya mila na desturi zake. Wizara inaendelea na utaratibu wa kukusanya maeneo ya kihistoria ya jamii mbalimbali hapa nchini na kuyahifadhi kwa njia ya TEHAMA. Vitabu vya historia na maandiko hayo yanapatikana katika Ofisi za Idara ya Nyaraka za Taifa, maktaba pamoja na maduka mbalimbali ya vitabu nchini.