Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 51 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 433 2018-06-14

Name

Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI (K.n.y. MHE. OMAR A. KIGODA) aliuliza:-
Kumekuwa na utekelezaji hafifu wa kusaidia akinamama na vijana kutoka kwenye ile asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri:-
Je, Serikali ina tathmini yoyote ya jinsi gani agizo hilo limetekelezwa kwa kila halmashauri?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Omar Abdallah Kigoda, Mbunge wa Handeni, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali hufanya ufuatiliaji na tathmini kila robo mwaka, nusu mwaka na mwaka kuhusu utekelezaji wa agizo la kila Halmashauri kutenga asilimia 10 kwa ajili ya vikundi vya vijana na wanawake. Taarifa za ufuatiliaji na tathmini ndizo zimesaidia Serikali kubaini changamoto za usimamizi na uendeshaji unaotokana na upungufu wa kisheria, ikiwa ni pamoja na baadhi ya wanufaika wa mikopo kuwa wagumu kurejesha mikopo yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia Marekebisho ya Sheria ya Fedha ya mwaka 2018 yatakayompa Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa nguvu ya kutunga kanuni bora zaidi zitakazolazimisha halmashauri kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya mikopo ya akinamama na vijana, Serikali inaamini taratibu za utoaji wa mikopo hiyo, usimamizi na urejeshaji wake zitakuwa nzuri zaidi ukilinganisha na hali ilivyo sasa.