Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 42 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 357 2018-06-01

Name

Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. ALLY SALEH ALLY (K.n.y. MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN) aliuliza:-
Je, Chuo cha Utalii kimetoa wahitimu wangapi wa fani za hoteli za kitalii kwa mwaka 2016/2017?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa maliasili na utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yussuf Salim Hussein, Mbunge wa Chambani, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Chuo cha Taifa cha Utalii ni Wakala uliopo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii wenye dhamana ya kutoa mafunzo ya ukarimu na utalii nchini. Aidha, chuo kinatoa ushauri wa kitaalam na kufanya utafiti katika fani ya ukarimu na utalii. Chuo cha Taifa cha Utalii kina ithibati kutoka Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) ili kutoa mafunzo ya ukarimu, usafiri na utalii kwa ngazi za stashahada na astashahada.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa masomo 2016/2017 kupitia kampasi zake tatu za Bustani, Temeke Dar es Salaam na Sakina Arusha, kilitoa mafunzo ya ukarimu, usafiri na utalii kwa wahitimu 329 kama ifuatavyo:-
(a) Stashahada ya Usafiri na Utalii (Ordinary Diploma ni Travel and Tourism) wahitimu 43;
(b) Stashahada ya Ukarimu (Ordinary Diploma in Hospitality Operations) wahitimu 15;
(c) Astashahada ya Ukarimu (Technician Certificate in Hospitality Operations) wahitimu 78;
(d) Mafunzo ya Muda Mfupi (Short Courses in Food Production and Pastry and Bakery) wahitimu 78; na
(e) Mafunzo ya Uhitaji Maalum (Tailor Made Courses in Hospitality and Tourism) wahitimu 79.
Mheshimiwa Naibu Spika, mafunzo hayo yamekuwa yakitolewa kwa kutumia mitaala inayofuata Mfumo wa Kujenga Ujuzi na Maarifa (Competence Based Education and Training) inayosimamiwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE).