Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Primary Question

MHE. ALLY SALEH ALLY (K.n.y. MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN) aliuliza:- Je, Chuo cha Utalii kimetoa wahitimu wangapi wa fani za hoteli za kitalii kwa mwaka 2016/2017?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Swali la kwanza, Tanzania tunalenga kujiondoa kwa watalii 1,300,000 kwa mwaka na pia kujiondoa kwenye mchango wa utalii katika pato la Taifa kwa asilimia 17.5 na pia kufikia ajira milioni mbili zinazotokana moja kwa moja na utalii. Je, Serikali haioni kiwango cha diploma na certificate ni kidogo kwa sasa na kwamba tuende kwenye degree? Ni lini Serikali inajipanga kuongeza hadhi chuo hicho kiwe na uwezo wa kutoa degree?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, injini ya kutawala sekta ya utalii ni elimu na ujuzi katika eneo la menejimenti. Je, ni lini Serikali inapanga kuwezesha Chuo hicho cha Utalii kutoa course ya juu ya menejimenti ili kuondoa wageni kutawala sekta hii katika eneo la menejimenti? Ahsante.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Ally Saleh, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwamba mpaka sasa hivi tumekuwa tukitoa stashahada na astashahada lakini hivi sasa Serikali ina mpango wa kuanzisha degree katika maeneo hayo kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Columbia kutoka Canada. Baada ya kukamilika mitaala na ikishapitishwa, basi tutaanza kutoa hizo degree ambazo zitawaandaaa vijana wetu katika hizo fani ambazo Mheshimiwa Mbunge ameuliza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kuhusu masuala ya mafunzo ya menejimenti, ni kweli kabisa tumekuwa na changamoto kubwa katika mafunzo na course zinazotolewa kwa ajili ya menejimenti kuwaandaa vijana kuweza kushika nyadhifa mbalimbali katika hoteli zetu na katika maeneo mbalimbali. Hivi sasa Wizara kuanzia mwaka wa fedha 2018/ 2019 tunategemea kutoa mafunzo ya muda mfupi kwa watu mbalimbali, ambayo yatahusu watu zaidi ya 800 katika maeneo ya menejimenti ili kuwaandaa na kuweza kushika nyadhifa mbalimbali na nafasi katika utumishi katika maeneo ya utalii.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. ALLY SALEH ALLY (K.n.y. MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN) aliuliza:- Je, Chuo cha Utalii kimetoa wahitimu wangapi wa fani za hoteli za kitalii kwa mwaka 2016/2017?

Supplementary Question 2

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii. Najua nia ya Serikali ya kuanzisha vyuo hivi ni pamoja na kukuza utalii na kuingiza pato la letu la ndani na nje.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi sasa tembo wametoka kwenye Hifadhi ya Udzungwa National Park wameshambulia katika Vijiji vya Mailindi, Maghana kwenye Kata ya Mahenge, wananchi wako kwenye hali mbaya na jambo hili limekuwa likijitokeza kila mwaka. Naomba tu Mheshimiwa Waziri aende akaone hali jinsi ilivyo lakini pia ahakikishe kwamba kituo kidogo cha askari wa wanyamapori kinafunguliwa pale. Tatizo hili ni la kila mwaka, namwomba sana Mheshimiwa Waziri.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali ya Mheshimiwa Balozi Venance Mwamboto, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mwamoto, amekuwa akifuatilia sana hili suala na tumekuwa tukizungumza ni hatua gani ambazo tunaweza kuzichukua. Naomba nimhakikishie kwamba nitakuwa tayari kwenda kuangalia hali halisi katika Kata hiyo ya Mahenge ili kuona ni hatua gani zichukuliwe na Serikali. Moja ya hatua ambazo tunategema kuzichukua ni pamoja na kujenga out post katika lile eneo ili wasaidiane na wananchi na Halmashauri ile katika kudhibiti hao tembo ambao wamekuwa wakizagaa katika maeneo mbalimbali.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY SALEH ALLY (K.n.y. MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN) aliuliza:- Je, Chuo cha Utalii kimetoa wahitimu wangapi wa fani za hoteli za kitalii kwa mwaka 2016/2017?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, hawa wabeba mizigo kwenye milima yetu ambao wanatembeza Wazungu wamekuwa hawapewi mafunzo na wanafanya kazi hii kwa uzoefu Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha wanapatiwa mafunzo haya lakini na maslahi yao kwa ujumla yanatazamwa?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso ambalo kwa kweli anataka kujua kwamba ni mpango gani tulionao katika kutoa mafunzo kwa hawa wanaobeba mizigo. Naomba nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tumejiandaa vya kutosha katika mwaka huu wa fedha unaoanza Julai mwaka 2018, tunategemea kutoa mafunzo mafupi kwa hao watu wote pamoja na wale wanaongoza utalii katika eneo la Mlima Kilimanjaro ili kusudi waweze kutoa zile huduma ambayo wateja wetu wanazitarajia. Kwa hiyo, awe na subira, baada ya mwaka kuanza ataona matunda na mabadiliko makubwa yatakayojitokeza.