Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 55 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 366 2018-06-21

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:-
Serikali imeanzisha utaratibu wa kutoa elimu bure na kuanza kutekeleza utaratibu huo kwa kupeleka fedha shuleni kidogo kidogo kulingana na idadi ya wanafunzi husika tangu Oktoba 25, 2015:-
(a) Je, Serikali inafahamu kwamba shule nyingi za msingi na za sekondari nchini zikiwemo za Mtwara Mjini zilikuwa na madeni mengi ya wazabuni na steshenari?
(b) Je, Serikali inaweza kueleza kuwa madeni hayo yatalipwa kwa utaratibu upi ikiwa fedha zinazotolewa ni kidogo kwa uwiano wa mwezi kwa mwaka husika?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maftaha Abdallah Nachuma, Mbunge wa Mtwara Mjini lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua uwepo wa madeni katika shule za msingi na sekondari ambayo yanaanzia mwaka wa fedha 2008/2009 hadi 2016/2017, ikiwa ni madeni ya wazabuni kwa ajili ya chakula cha wanafunzi shuleni na shajara. Katika ya hayo, Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani inadaiwa shilingi milioni 92.4. Madeni hayo ni yale yalikuwepo kabla ya kuanza kwa utekelezaji wa Mpango wa Elimu bila Malipo Desemba, 2015. Kwa sasa, Serikali imejizatiti kutozalisha madeni, ambapo fedha za chakula na mahitaji mengi zinapelekwa kwenye kila shule moja kwa moja kila mwezi. (Makofi)