Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 57 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 480 2018-06-25

Name

Issa Ali Abbas Mangungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ISSA A. MANGUNGU aliuliza:-
Serikali ilikuwa na utaratibu wa kutoa Posho ya Kufundishia (Teaching Allowance) lakini kwa sasa imefutwa:-
(a) Je, ni kwa nini Serikali iliifuta posho hiyo?
(b) Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kuirejesha posho hiyo?
(c) Katika Jimbo la Mbagala, shule nyingi hazina nyumba za walimu; mfano, Shule za Msingi Mbagala, Maji Matitu na Rangi Tatu. Je, ni lini Serikali itatatua kero hii kwa mkakati maalum kama ilivyoweka mkakati wa upatikanaji wa madawati?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Issa Ali Mangungu, Mbunge wa Jimbo la Mbagala, lenye sehemu (a), (b) na (c) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali haikufuta Posho ya Kufundishia bali iliijumuisha katika mshahara wa mwalimu kwa lengo la kuongeza kiwango cha fedha (pensheni na kiinua mgongo) baada ya kustaafu. Awali posho hiyo ilikuwa inatolewa kwa watumishi nje ya mshahara, hivyo, haikuwa sehemu ya kikokotoo cha mafao ya watumishi baada ya kustaafu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua upungufu wa nyumba za walimu uliopo katika maeneo yote mijini na vijijini. Hata hivyo, kutokana na urahisi wa walimu na watumishi wengine wa Serikali kupata nyumba za kupanga maeneo ya mjini kama ilivyo katika Manispaa za Jiji la Dar es Salaam, kipaumbele cha juu cha ujenzi wa nyumba za walimu kimewekwa zaidi katika maeneo ya vijijini kule ambako kuna mazingira magumu ya kupata nyumba za kupanga ili kuboresha mazingira ya kufanyia kazi kwenye maeneo hayo.