Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Ali Abbas Mangungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ISSA A. MANGUNGU aliuliza:- Serikali ilikuwa na utaratibu wa kutoa Posho ya Kufundishia (Teaching Allowance) lakini kwa sasa imefutwa:- (a) Je, ni kwa nini Serikali iliifuta posho hiyo? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kuirejesha posho hiyo? (c) Katika Jimbo la Mbagala, shule nyingi hazina nyumba za walimu; mfano, Shule za Msingi Mbagala, Maji Matitu na Rangi Tatu. Je, ni lini Serikali itatatua kero hii kwa mkakati maalum kama ilivyoweka mkakati wa upatikanaji wa madawati?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA A. MANGUNGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa Serikali inasema kwamba wameingiza Teaching Allowance katika mishaharana Serikali ilikuwa inafanya uhakiki kwa ajili ya kulipa madeni ya walimu na malimbikizo yao wakati wa kustaafu na wale ambao wako kazini. Je, Serikali imefikia wapi katika kuhakiki madeni hayo na kuyathibitisha ili walimu sasa waanze kulipwa maana wamekuwa wakisumbuka na muda mrefu wamekosa kupata haki zao hasa wale waliostaafu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, anasema kwamba walimu wa mijini wanaweza wakapanga nyumba. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuwaongezea allowance hizi ili waweze kukabiliana na changamoto ya nyumba katika maeneo ya mijini? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Issa Ali Mangungu, Mbunge wa Mbagala, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, napenda nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako Tukufu kwamba Serikali imeshakamilisha uhakiki wa madeni na watumishi wengi tu wakiwemo walimu wameshaanza kulipwa. Wale ambao hawajalipwa naomba waendelee kusubiri, muda wao wa kulipwa ukifika watalipwa. Hakuna mtu yeyote ambaye hatalipwa deni ambalo ni halali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili ameuliza kwamba Serikali ina mpango gani wa kuwaongezea allowance walimu? Napenda nimhakikishie kwamba Serikali ni mwajiri wa watumishi wote, siyo walimu peke yake. Kwa hiyo, kama ambavyo tumeweka utaratibu mzuri wa kuhakikisha kwamba tunaweka kipaumbele cha kuwa na nyumba katika maeneo ambayo ni vigumu kupata nyumba kama maeneo ya vijijini ambako hakuna hata nyumba za kupanga kwa watumishi wote; watumishi wa afya, walimu na watumishi wengine, hivyo hivyo hatuwezi kubagua kwamba sababu ni walimu kwa sababu ni walimu, tuwaongezee allowance walimu peke yao watumishi wengine tuwaache gizani, hapana. Nadhani huo utakuwa ni ubaguzi na Serikali haiwezi kufanya hivyo.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ISSA A. MANGUNGU aliuliza:- Serikali ilikuwa na utaratibu wa kutoa Posho ya Kufundishia (Teaching Allowance) lakini kwa sasa imefutwa:- (a) Je, ni kwa nini Serikali iliifuta posho hiyo? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kuirejesha posho hiyo? (c) Katika Jimbo la Mbagala, shule nyingi hazina nyumba za walimu; mfano, Shule za Msingi Mbagala, Maji Matitu na Rangi Tatu. Je, ni lini Serikali itatatua kero hii kwa mkakati maalum kama ilivyoweka mkakati wa upatikanaji wa madawati?

Supplementary Question 2

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Utakubaliana nami kwamba hakuna kada inayonyanyasika hapa nchini kama walimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni Serikali ilipunguza baadhi ya walimu wa sekondari kwenda shule za msingi kutokana na upungufu wa walimu na ikadai kwamba ina fedha za kuwalipa. Leo tunavyozungumza, baadhi ya Wakurugenzi wamewaambia wale walimu warudi kwenye shule za sekondari. Kwa hiyo, ina maana Serikali ilikuwa haijajipanga. Je, ni lini Serikali itawalipa walimu hao fedha kama ambavyo walidai kwamba watawalipa?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Susan Lyimo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza uamuzi ule wa kuhamisha walimu wa sanaa waliozidi katika shule za sekondari kuwapeleka kwenye shule za msingi ulikuwa ni sahihi. Kilichosisitizwa ni kwamba mtumishi yeyote anastahili apate haki zake kama ilivyoainishwa kwenye Kanuni zetu za Utumishi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, tangazo la Mheshimiwa Rais limetoka mwezi Februari kwamba mtumishi asihamishwe mpaka alipwe, wale ambao walikuwa wameshahamishwa watalipwa madeni yao halali, wala hakuna tatizo. Wale ambao walikuwa bado, wasubiri, watahamishwa baada ya fedha kupatikana. Wale ambao wamerudishwa ni kwa muda tu. Kwa hiyo, naomba hili liwe clear wala halina matatizo yoyote.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. ISSA A. MANGUNGU aliuliza:- Serikali ilikuwa na utaratibu wa kutoa Posho ya Kufundishia (Teaching Allowance) lakini kwa sasa imefutwa:- (a) Je, ni kwa nini Serikali iliifuta posho hiyo? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kuirejesha posho hiyo? (c) Katika Jimbo la Mbagala, shule nyingi hazina nyumba za walimu; mfano, Shule za Msingi Mbagala, Maji Matitu na Rangi Tatu. Je, ni lini Serikali itatatua kero hii kwa mkakati maalum kama ilivyoweka mkakati wa upatikanaji wa madawati?

Supplementary Question 3

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika imejitahidi sana kuhamasisha wananchi kujenga vyumba vya madarasa na nyumba za walimu lakini bado kunahitajika nguvu ya Serikali kumalizia majengo yale ikiwemo Shule ya Msingi Busongola, Bulamata, Pandandogo na nyinginezo. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha hizo ili ziweze kumalizia majengo hayo ambayo wananchi wamejitolea? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Moshi Selemani, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa, kwa nchi nzima maeneo mengi kabisa wananchi wamejitahidi, wamejenga majengo na mengi ya majengo hayo yamefika kwenye lenta tayari kumaliziwa. Sasa hapo ni jukumu letu sisi Serikali, Halmashauri na wadau wengine kuunga mkono nguvu za wananchi. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba suala hilo tunalizingatia. Naomba sana tuwasiliane mwezi huu wa Julai na Agosti ili kusudi tuweze kuyatatua matatizo kama hayo.